Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

‘PADRI’ AKAMATWA KWA TUHUMZA ZA KUMCHINJA MFANYABIASHARA MKOANI ARUSHA

Na Woinde Shizza

Mtuhumiwa mauaji ya kutisha ya kumkata viungo vya mwili marehemu zikiwemo sehemu za siri, viganja vya mikono na matiti mauaji yaliotokea kwenye hotel ya A Square Belmot amekamatwa na jeshi la polisi mkoani hapa.


Akiongea na vyombo vya habari ofisini kwake kamanda wa polisi, Naibu kamishna wa jeshi la polisi mkoani hapa Liberatus Sabas alisema kuwa mtuhumiwa alikamatwa juzi majira ya asubuhi katika eneo la TRA House jijini hapa.


Sabas alisema kuwa alipohojiwa na polisi alikiri kushiriki mauaji hayo na ndipo alipowapeleka kuwaonyesha polisi alipovitupa viungo vya marehemu eneo la mto misheni usa river nje wilayani meru.


Alisema kuwa marehemu ametambuliwa jina kamili Alfred Kimbaa mwenye umri wa miaka18 mkazi wa mianzini jijini hapa huku mtuhumiwa ambaye jina lake limetambuliwa kwa Elijus Lyatuu mkazi wa Dar es Salaam ambaye marehemu alikuwa akiuza duka la kaka yake alietambuliwa kwa jina moja la Lyatuu anaeishi jijini Dar es salaam.


Alisema kuwa mtuhumiwa ni mwanafunzi wa mwaka wa tano chuo cha falsafa cha kanisa katoliki Segerea na alipofika Arusha kwa mara ya kwanza aliishi na marehemu chumba kimoja kabla ya mgogoro kuanza na ndipo alipofikia kumuua marehemu na kuiacha maiti yake katika hotel nae kutokomea kusikojulikana hadi alipokamatwa juzi.


Alisema kuwa mtuhumiwa Elijus alimua marehemu kwanza kabla ya kuanza kucharanga viungo ndio maana chumbani alikokutwa marehemu hakukua na damu.


“Tukio hili lisihusishwe na imani za kishirikina kwani kulikuwa na mgogoro kati ya mtuhumiwa na marehemu uliopelekea mtuhumiwa kufanya tukio hilo”alisema Kamanda Sabas


Upelelezi ukikamilika na taratibu za jeshi la polisi zinaendelea na zikikamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.

STORI NA: LIBENEKE LA KASKAZINI

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO