Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

ARSENAL YAANZA VIBAYA EPL NI BAADA YA KUCHARAZWA 2 KWA MTUNGI NA WESTHAM UNITED

Klabu ya Arsenal imeanza vibaya msimu mpya wa Ligi Kuu ya England baada ya kuchapwa mabao 2-0 na West Ham United Uwanja wa Emirates jioni ya leo.

Cheikhou Kouyate alianza kufunga akitumia makosa ya kipa Petr Cech kuipatia West Ham bao la kwanza dakika ya 43, kabla ya Mauro Zarate kufunga la pili dakika ya 57.

Adrian aliokoa michomo kadhaa ya hatari katika mchezo ambao kocha Slaven Bilic alimtumia kinda wa miaka 16, Reece Oxford akicheza mechi yake ya kwanza ya Ligi Kuu England.


Kikosi cha Arsenal; Cech, Debuchy/Sanchez dk67, Mertesacker, Koscielny, Monreal, Coquelin/Walcott dk58, Cazorla, Ramsey, Ozil, Oxlade-Chamberlain na Giroud.

West Ham: Adrian, Tomkins, Reid, Ogbonna, Cresswell, Oxford/Nolan dk79, Noble, Kouyate, .Payet, Zarate/Jarvis dk63, Sakho/Maiga dk89

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO