Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

UJUE WASIFU WA MHE. EDWARD LOWASSA, MGOMBEA URAIS WA USHIRIKIANO WA UKAWA

 


WASIFU WA MHE. EDWARD LOWASSA:
Edward Ngoyai Lowassa alizaliwa tarehe 26 August 1953, katika kijiji cha Ngarash wilayani Monduli mkoa wa Arusha, akiwa ni mtoto wa 4 kati ya watoto 23 wa mzee Ngoyai Lowassa.
Edward Lowassa amemuoa Regina Lowassa na kujaliwa kupata watoto watano, watatu wakiume na wawili wa kike.
ELIMU:
1961 - 1967: shule ya msingi Monduli
1968-1971: shule ya sekondari Arusha
1972 - 1973: St. Marry's High School (Milambo High School) Tabora.
1983 - 1984: Chuo Kikuu cha BATH Uingereza M.Sc (Development Studies).
UZOEFU KAZINI:
1977-1978: Katibu Msaidizi ccm mkoa wa Shinyanga
1979-1982: Katibu Mtendaji ccm mkoa wa Arusha.
1983-1985 - Katibu mkuu msaidizi ccm Mkoa wa Kilimanjaro.
1985-1995 - Mbunge wa umoja Vijana wa ccm.
1989-1990 - Mkurugenzi Mtendaji Kituo cha mikutano cha kimataifa (AICC) Arusha.
1990-1993 - Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu na makamu wa kwanza wa rais anayeshughulikia sera, Uratibu Bunge, Maafa namasuala ya mahakama.
1993-1995 - Waziri wa Ardhi, nyumba na maendeleo ya miji.
1995-2005 - Mbunge wa Monduli (ccm)
1995 - 2000 - Waziri nchi ofisi ya makamu wa Rais Mazingira, Muungano nakuondoa umasikini.
2000 -2005 - Waziri wa maji na maendeleo ya mifugo.
Desemba 2005 Februari 2008 Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
1985 - 2005 - Mbunge wa Monduli (ccm)
2010 - 2011 - Mwenyekiti Kamati ya bunge ya ulinzi na usalama na mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa .
2011 - 2015 - Mwenyekiti kamati ya bunge ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa.
28/07/2015 - Kujitoa CCM na kujiunga na CHADEMA
Mhe. Edward Lowassa ni shabiki wa michezo na alikuwa mchezaji mzuri wa mpira wa kikapu

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO