Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Rais Kikwete aungana na viongozi wa Afrika kutofurahia Mahakama ya ICC kuwashughulikia waafrika zaidi!

in3

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifungua Mkutano wa 16 wa mwaka wa Chama Cha Wanasheria wa Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika SADC uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere(JNICC) jijini Dar es Salaam leo. (picha na Freddy Maro)
*****
Katika kile ambacho kwa wakati huu kinaweza kuonekana kama kumshtua Rais Kikwete ni hatua yake ya kurejea kauli ambayo imekuwa ikitolewa na viongozi wa Afrika dhidi ya Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC) kwamba viongozi wengi wa Afrika hawafurahii namna Mahakama hiyo inavyofanya kazi zake kwa kuwashughulikia viongozi wa mataifa ya Afrika. Rais Kikwete alirudia kauli hiyo jana wakati akifungua Mkutano wa 16 wa Wanasheria wa SADC.
 Mtanzania, Agosti 22, 2015 linaripoti

Hii ni mara ya pili katika muda wa wiki moja Mahakama hiyo inazungumzwa na viongozi wa kubwa wa kisiasa nchini.
Mara ya kwanza ilikuwa ni Agosti 15, 2015 Jijini Arusha katika viwanja vya Tindigani-Kimandolu ambapo kulikuwa na mkutano mkubwa wa mgombea wa CHADEMA kwa nafasi ya urais Mh Edward Lowassa akiwakilisha vyama vinavyounda ushirikiano wa kisiasa UKAWA, akitafuta wadhamini aliitahadharisha Serikali kutoendelea kuwatendea visivyo raia wasiokuwa na hatia.

Lowassa alikuwa akizungumzia madhila yaliyoukumba msarafa waka siku moja kabla akielekea msibani na siku hiyo ya mkutano ambapo Polisi walitumia mabomu ya machozi kujaribu kuutawanya msafara wake uliokuwa unatokea KIA kuelekea eneo la mkutano Kimandolu, Arusha.

Akasema alivyokuwa Serikalini alikuwa akisikia tu kuwa wapinzani wanapigwa na Polisi bila sababu lakini sasa amejua. Akaongezea kuwa Serikali ikiendelea na matendo hayo ataandikisha jina lake kwenye Mahakama hiyo ya ICC.

Hatuna uhakika kama maelezo haya ya Lowassa yanauhusiano wowote na kauli ya Rais jana.

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO