Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Msafara wa Lowassa kwenda msibani kwa Mzee Kisumo wazuiwa na Polisi Mwanga!

Lowassa na msafara wake wa makumi ya wafuasi wa ushirikiano wa vyama vinne maarufu kama UKAWA wamejikuta wakishindwa kuendelea na safari ya kumsindikiza Mgombea wa Urais kupitia CHADEMA, chama mshirika wa umoja huo Mh Edward Lowassa kuhudhuria sherehe za maziko ya Maehemu Mzee Peter Kisumo na kurejea Mjini Moshi.

Baadhi ya viongozi alioambatana nao Mh Lowassa na wote wamerudi baada ya kuziiwa ni pamoja na Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, Mh James Mbatia, Mbunge wa Rombo Mh Joseph Selasini, Mbunge aliyemaliza muda wake Moshi Mjini Mh Philemon Ndesamburo na viongozi wa Mkoa na Wilaya.

Kwa mujibu wa mtoa taarifa, tukio hilo limetokea mchana wa leo eneo la Kijiji cha Maroro Wilayani Mwanga ambapo askari wa Jeshi la Polisi kwa kutumia magari yake na rilaha za moto na mabomu ya mwachozi walitanda badarabari kuzuia msafara huo usiweze kuendelea.

Blogu hii haijaweza kupata sababu hasa zilizopelekea Jeshi la Polisi kuamua uamuzi huo kuwazuia watu waliokuwa wnakwenda kwenye msiba wa Mzee Kisumo. Hata hivyo dodoso za hapa na pale zinaeleza tetesi kuwa askari hao wametekeleza tu maagizo ya wakubwa wao.

Baadhi wa askari wakionekana kudhibiti eneo la barabara huku wanahabari wakiendelea kukusanya matukio
Mjumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mapokezi ya Mh Edward Lowassa Kanda ya Kaskazini, ambaye pia ni mwania Ubunge Jimbo la Same Magharibi Mh Christopher Mbajo (mwenye kombati nyeusi) akiwa hajui hili wala lile baada ya msafara wao kuzuiwa katika Kijiji cha Maroro.
Kiongozi wa brigedia ya ulinzi na usalama CHADEMA
 
 
Askari wakiwa tayari kuukabili msfara huo
Bdoboda wakiwa hawana namna baada ya msafara wao kuzuiwa
 
Maroro
Kijana aliyeshinda Kura za Maoni Jimbo la Mkalama CHADEMA, Oscar Kapalale akifuatilia jambo
PICHA ZOTE NA: CHRIS MBAJO
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO