Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

LOLIONDO KWALIPUKA TENA…. MWANDISHI WA BBC AKAMATWA; MWIGULU NCHEMBA AHUSISHWA

Mida ya jioni kama saa kumi na mbili kasorobo  Mwandishi wa Habari wa BBC  Bw. Jayson amekamatwa Loliondo kwenye mkutano uliododa wa Mwigulu Nchemba uliopo kata ya Waso.

Inasemekana mwandishi huyo alikamatwa baada ya kugundulika alikuwa anafanya uchunguzi kuhusu migogoro kati ya Wamasai wa Loliondo na Mwaarabu anayejulikana kwa jina la Ortelo. Kwenye mkutano huo wamama wa kimasai walimrushia Mwigulu kadi za ccm huku wamepandwa na hasira.

taarifa zinaeleza zaidi kuwa, ilipo fika mida ya moja kasorobo Tundu Lissu aliweza kuombea  mwandishi wa BBC aliyekamatwa Bw. Jayson, Tundu Lissu ambaye naye alikuwa na mkutano huko ameamua kutoka Soitsambu kwenda kumtetea na kuhoji sababu za mwandishi wa habari kukamatwa.

Waandishi wengine wa habari Ramadhan Mvungi wa Startv na Musa Juma inasadikiwa wamekimbilia porini baada ya Mwigulu kuagiza wakamatwe, akihoji nani aliwaita kwenye mkutano wake!

Chanzo: Media 2 Solution

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO