Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Taswira: Makamu wa Rais Dkt. Bilal Akihitimisha Matembezi ya Wahandisi jana

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akishiriki katika matembezi ya hisani ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kujenga uwezo wa Wahandisi wa Tanzania, yaliyoandaliwa na Wahandisi hao (Local Engineers). Matembezi hayo yalianzia katika Viwanja vya Karimjee jijini na kumalizikia katika Viwanja vya Leaders Club Kinondoni, jijini Dar es Salaam, leo Oktoba 7, 2012.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Moahammed Gharib Bilal,akimkabidhi cheti, Mhandisi Grace Beo, kutoka Kampuni ya Temesa ICT Engineer, akiwa ni mmoja kati ya waliochangia na kushiriki vyema katika zoezi la kuchangisha fedha kwa ajili ya kujenga uwezo wa Wahandisi wa Tanzania, yaliyoandaliwa na Wahandisi hao (Local Engineers). Makamu alikabidhi vyeti hivyo baada ya kuhitimisha rasmi matembezi hayo ya hisani yaliyoanzia katika Viwanja vya Karimjee na kumalizikia kwenye Viwanja vya Leaders Club Kinondoni jijini Dar es Salaam, leo Oktoba 7, 2012.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu na Wahandisi (Local Engineers) baada ya kuhitimisha matembezi hayo katika viwanja vya Leaders Club Kinondoni, jijini Daar es Salaam leo, Oktoba 7, 2012.

Picha na Muhidin Sufiani-Ofisi ya Makamu wa Rais

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO