Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

IMF Ipunguze Masharti Ya Mikopo-Mgimwa

Waziri wa Fedha Mhe William Mgimwa akitoa maelekezo kwa Msemaji wa Wizara ya Fedha Bi. Ingiahedi Mduma, Kamishina Msaidizi wa Fedha za Nje Bw. Jerome Bureta na Afisa mwandamizi Bw. Omary Khama Jijini Tokyo-Japan

Waziri wa Fedha Mhe. William Mgimwa akijadiliana na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Bw. Harry Kitilya, Mkurugenzi Utafiti Uchumi na Sera Dk.Joseph Leina Masawe wa Benki Kuu ya Tanzania, Ofisa Mwandamizi Bw. Omary Khama na Bw. Cyprian kuyava wa Wizara ya Fedha baada ya mikutano hiyo ya IMF kwa siku ya leo hapa Jijini Tokyo- Japan.

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA FEDHA

MGIMWA ALISHAURI SHIRIKA LA FEDHA LA KIMATAIFA KUPUNGUZA MASHARTI YA MIKOPO

INAYOKOPWA NA NCHI ZINAZOENDELEA.

“Shirika la fedha la kimataifa (IMF) hujishughulisha na kutoa ushauri wa kisera kwa nchi wanachama na kutoa mikopo na misaada ya kifedha. Hayo yamesemwa na Mhe. Mgimwa jijini Tokyo- Japan. Akishiriki kikao cha kundi la Africa (African Group one Constituency),aidha,

Mheshimiwa Mgimwa aliwasilisha hoja kwa niaba ya Magavana wa Afrika, na mbele ya Naibu Mkurugenzi Mkuu wa IMF Bwana Shinowara, ya kulitaka shirika hilo kupunguza kiwango cha kigezo cha kukopa ili kuruhusu Nchi zinazoendelea kupata unafuu na kuziwezesha kukopa fedha za kufadhili kwa miundombinu ya Barabara, Reli na Bandari.

Mhe. Mgimwa alisema kuwa, mkutano huo uliangalia uhalisia na vigezo vinavyotolewa na Shirika la Fedha la kimataifa kuruhusu nchi wanachama kukopa tu katika ukomo wa sasa wa asilimia 35 na zaidi (Concesionality). Aliendelea kufafanua kwamba, jambo kubwa ni kuangalia jinsi ya kuboresha taratibu za kukopesha katika mikopo nafuu. Aidha, wajumbe wa mkutano wamekubaliana na haja ya kuwepo kwa utaratibu wa kuhakikisha kuwa nchi zote zinakuwa na madeni yanayohimilika”. Alisisitiza Mgimwa.

Wakijadiliana katika mkutano huo wajumbe hao wameshauri Shirika la fedha la kimataifa pamoja na taratibu zake, liangalie namna ya kulegeza masharti ya mikopo ili nchi wanachama ziweze kuboresha miundombinu.

“ IMF walau itizame aina ya miradi yenye chachu ya ukuwaji wa uchumi ambayo inaweza kutizamwa kwenye viwango vya ukopaji vya chini ya asilimia 35”.Aliongeza Mgimwa.

“Tunashukuru kuwa IMF imekuwa ikitupatia mikopo ya masharti nafuu, mikopo ile ya mapumziko ya miaka saba kabla ya kuanza kulipa na yenye riba ndogo sana na yenye masharti

Akitolea mfano wa mradi wa gesi wa Tanzania, Mgimwa alisisitiza kuwa upatikanaji wa gesi utaongeza uzalishaji, ajira na viwanda. Kuongezeka kwa ajira kutaongeza kukua kwa pato la Taifa. Hii itasaidia kuleta mabadiliko makubwa ya kiuchumi kwa nchi ya Tanzania na hata

Mikutano hiyo bado inaendelea hapa jijini Tokyo-Japan na nchi wanachama wanaendelea kuja

Imetolewa na Msemaji Mkuu -Wizara ya fedha
Bi. Ingiahedi Mduma
Tokyo-Japan
9 Oktoba 2012

IMEKUJIA KWA HISANI YA MJENGWA BLOG

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO