Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Mkutano wa waTanzania wanaoishi Ujerumani na Wafadhili kufanyika Jumapili 28-10-2012, Mjini Mainaschaff

UNION OF TANZANIANS IN GERMANY (UTU)
KUKUTANA NA WAFADHILI NA WAHISANI ZAIDI YA 150 !!!!

WORLD MISSION SUNDAY 28.OCT. 2012

UTU LogoUmoja wa Watanzania Ujerumani (UTU)  Unapenda kuwakaribisha Watanzania wote wanaoishi ujerumani, Katika Hafla ya WORLD MISSION SUNDAY. itakayofanyika Katika ukumbi Uliopo Hauptstr. 30, D-63814 Mainaschaff Jirani sana na Mji wa Aschaffenburg Siku ya Jumapili Tarehe 28.10.2012, Kuanzia saa 04:00  za Asubuhi. Ambapo Wasamaria wema na Wafadhili wapatao zaidi ya 150 kutoka sehemu mbali mbali za ujerumani watakutana na umoja wa Watanzania Ujerumani (UTU) Juu ya kuitakia mema Tanzania na kuanzisha Harambee ya kuchangia maendeleo ya miradi mbali mbali itakayosimamiwa na Umoja wa watanzania Ujerumani (UTU).

Katika Hafla hiyo Kuanzia saa  9 mchana watayarishaji wa Hafla hiyo ''World Mission Sunday'' itatoa nafasi kwa Umoja wa Watanzania Ujermani (UTU) Kuitambulisha Tanzania Kwa wahisani hao , na kuelezea ni mradi gani unahitaji  ufadhili kupitia Umoja huu.  Mmoja wa wageni rasmi walio alikuwa ni Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Mhe. Ahmada Ngemera, Dr. Lippert na mkewe Kutoka Scheinfurt' Dr. Lippert ni mtaalamu ambaye aliwahi kufanya kazi Tanzania. Hafla hii inategemewa kuisha saa 12:00 za jioni, baada ya hapo watanzania watapata muda wao wa kufanya mazungumzo na Mhe: Balozi wa Tanzania Nchini ujerumani Bw. Ahmada Ngemera.

Umoja wa Watanzania Ujerumani  UTU Umeramba Bingo kwa kupewa nafasi hii ya pekee  Na WORLD MISSION SUNDAY Kuiwakilisha Jamii ya watanzania na kuwashawishi Wafadhili na wahisani nchini ujerumani ili waweze kuchangia Miradi mbali mbali ya Huduma za jamii nchni Tanzania ikiwemo sekta ya Elimu na Afya.

Tunawaomba Watanzania Wote  na marafiki wa Tanzania  wanaoishi Ujerumani na jirani mwa ujerumani, kuhudhuria kwa wingi katika Hafla hii muhimu kwa jamii ya watanzani kama wasemavyo wahenga ''CHEREKO CHEREKO NA MWENYE MWANA'' Kwa maelezo zaidi wasiliana na kamati.utu@googlemail.com au unaweza kuwasiliana na Mwenyekiti Wa UTU moja kwa moja kupitia simu ya mkononi. 0173-4298997

Karibuni sana ! Umoja Ni Nguvu

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO