Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Sugu aahidiwa pikipiki 116 za M4C na wanaCHADEMA waishio Houston Tx Marekani; kuwa mgeni rasmi mkutano mwingine wa CHADEMA Boston Septemba 8

IMG-20120824-WA0004

Mbunge wa Mbeya Mjini (CHADEMA) Mh Joseph Mbilinyi almaarufu Sugu ambae bado yuko nchini Marekani na Mwenyekiti wa chama chake taifa Mh Freeman Mbowe kwa shughuli za chama anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye tukio lingine la cham hicho kama tangazo hili linavyoeleza.
Kwa mujibu wa maelezo ya Sugu kupitia akaunti yake ya Facebook amewashukuru wanaCHADEMA waishio Houston Texas Marekani kwa kujitolea pikipiki 126  kwa ajili ya kusaidia kusambaza harakati za CHADEMA kama sehemu ya ushiriki wao kuiondoa CCM madarakani ifikapo Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Uzinduzi wa tawi la Houston Texas

Juzi tarehe 25 August 2012 jijini Houston, Texas nchini Marekani Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kilifungua tawi lingine la pili tarehe  baada ya kufungua tawi  la awali Jijini Washington DC tarehe 27 MAY 2012, ikiwa ni muendelezo wa kufungua matawi mbalimbali nchini humo.

Sherehe hiyo ya Ufunguzi wa Tawi la Chadema Houston imehudhuriwa na Mwenyekiti wa Chadema Taifa Mhe Freeman Mbowe na Mbunge wa Mbeya mjini Mhe Joseph Mbilinyi "Sugu".

Viongozi wengine waliohudhuria ni Katibu wa Chadema Tawi la Washington DC Mhe Isidory Lyamuya na aliyekuwa katibu wa Kwanza wa Chadema Washington DC Mhe Liberatus Mwang'ombe.

Sherehe hizo ambazo zilifanyika katika Hotel ya Marriot zilihudhuriwa na Watanzania wengi waishio Houston. Katika Sherehe hizo wanachama wengi waliamua kujivua gamba na kuvaa Gwanda kama ishara ya kutaka kulikomboa Taifa la Tanzania linalozama katika Bahari ya Mafisadi.

Akiongea katika mkutano huo Mwenyekiti wa Chadema Houston Ndugu Fuefue ameahidi kufanya mambo makubwa kwa kushirikiana na wanachadema wa Houston na wapenda mabadiliko wote kuchangia kwa hali na mali katika operesheni inayoendelea hivi sasa ya M4C. Viongozi hao wa Chadema Houston wameahidi kuchangishana pesa ili kununua gari litakalosaidia katika operesheni ya M4C, pamoja na ahadi ya kutoa pikipiki 116 kama mchango wao kwa Chama kwa ajili ya M4C.

Taswira mbali mbali zikionesha matukio ya  uzinduzi wa tawi la mjini Houston Texas, Marekani. Picha na maelezo kwa hisani ya (Chadema Blog)
Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO