Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

WADAU WA MAJI ARUSHA WAKUTANA KUJADIL KUPANDA KWA MAJI

Wadau wa maji waliofika katika mkutano huo

Mkurugenzi wa AUWSA, Eng.Ruth Koya akiwa anasoma maoni kwa watumiaji maji jana jijini Arusha mkutano ulioshirikisha wadau mbalimbali wa maji

****

Mjumbe wa baraza la watumiaji wa huduma zinazodhibitiwa na EWURA(EWURA CCC) Bi..Mayrose Kavura Majinge alisoma maoni  ya baraza  hilo na kusema katika wasilisho la mamlaka kunamkanganyiko wa taarifa mbalimbali zilizoonyesha kukosekana umakini au upotoshwaji wa maksudi wenye lengo la kuhaalisha maombi ya kupandisha bei ya huduma yamaji

Aidha alibainisha kuwa  katika Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi wa hesabu ya Serikali ya mwaka ulioisha June 2011 inaonyesha ufanisi mdogo wa kiutendaji hivyo inaonekana asilimia kubwa ya watumiaji wa maji hawalipi huduma hiyo hivyo kupandisha bei kutamuumiza mwananchi

Akifungua Taftishi hiyo mkuu wa wilaya ya Arusha John Mongela kwa niaba ya RC wa mkoa huu alisema kuwa

Watumiaji,wadau wa huduma ya  maji wanao wajibu wa kulipia huduma ya maji kwani haki bila wajibu ni vurugu,na wajibu bila haki ni utumwa hivyo wanao wajibu wa kulipia huduma hizo kikamilifu na kwa wakati

Bw.Mongela alisema kuwa AUWSA wanawajibu pia wa kuwapa huduma iliyosahihi watumiaji wahuduma hiyo na kuacha kutumia njia hiyo kuwakandamiza wananchi kwani kukosa huduma kwa mwezi halafu unalipia huo utakuwa ni wizi na kuwarudisha nyuma wananchi.

Naye mkazi wa jijini hapa Bw. Alli Iddy akichangia hoja, aliwataka AUWSA kutafuta wawekezaji wa maji ili tatizo la uhaba wa maji hapa Mkoani lipatiwe ufumbuzi zaidi ya kupandisha bei ya maji

SOURCE: JAMII BLOG “Pmela Mollel”

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO