Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Taarifa Fupi kuhusu Kazi za Maendeleo Jimboni Ubungo (AMUA)

UTANGULIZI:

Kwa nyakati mbalimbali kumekuwepo na mijadala kwenye mitandao ya kijamii kuhusu utendaji kazi wangu katika kuwezesha maendeleo Jimboni Ubungo. Mijadala hiyo imeshika kasi jana tarehe 20 Agosti 2012 siku nzima baada ya habari kwenye ukurasa wa mbele wa gazeti la Tanzania Daima “Mnyika kinara bungeni” ambayo imerejea rekodi za bunge na kuniweka katika orodha ya wachangiaji wa mara kwa mara bungeni.

Napokea kwa unyenyekevu pongezi zilizotolewa na wachangiaji mbalimbali lakini izingatiwe kuwa michango yangu bungeni ni matokeo ya heshima mliyonipa ya kuwawakilisha. Aidha yapo maoni machache ambayo yametoa tafsiri tenge kuhusu kazi ya mbunge na wengine mmetaka nieleze nimefanya kazi gani za maendeleo jimboni Ubungo.

Tarehe kama ya leo 21 Agosti 2005 nilianza mchakato wa kuwa kugombea ubunge nikiwa kwenye chakula na watoto yatima, tarehe kama hiyo mwaka 2010 nilianza kampeni za uchaguzi mitaani Ubungo, tarehe hii hii kwa mwaka huu wa 2012 naomba niitumie kutoa taarifa fupi ya utekelezaji kwa masuala ya maendeleo katika mwaka wa fedha 2011/2012 uliomalizika tarehe 30 Juni 2012; taarifa ya kina ya utekelezaji nitaitoa nitakapotimiza miaka miwili ya utendaji.

AHADI NILIZOTOA WAKATI WA UCHAGUZI WA MWAKA 2010

Kabla ya kueleza kazi nilizofanya katika kutimiza majukumu ya kibunge katika kuwezesha maendeleo jimboni ni muhimu nikawapa rejea ya ahadi nilizotoa wakati wa uchaguzi wa mwaka 2010 ili kupata msingi  wa kupima utekelezaji.

KONG’OLI HAPA KUSOMA TAARIFA KAMILI

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO