Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Utenzi wa Mashaka Mgeta kuhusu anguko la CCM na Dr Kafumu Igunga

Kafumu amevuliwa ubunge,

Makosa Ya 'wahafidhina' wa CCM,

Wale wasioyaona mabadiliko,

Wasiotaka kuyaishi mabadiliko,

Wasioyakubali mabadiliko.

 

Wamefanya 'uvundo wa kisiasa',

Wameukasirisha umma,

Wameumbuliwa na Mahakama,

Pole sana Kafumu!

Pole sana mwana mawasiliano mwenzatu.

 

Kwa jeuri na ulevi wa madaraka,

Wasiostahili, wamekusababishia usichostahili.

Hukumu imeshatoka,

Taji la ubunge umevuliwa,

Mjengoni hawatakuona,

Pumzika, anza upya.

 

Ole wako CCM,

Ole kwa jeuri ya waliomo ndani yako,

Wakitumia rasilimali za umma,

Wanakiuka yaliyo ya umma.

 

Wanajivisha jeuri ya kutoguswa,

Wafanye wanalolitaka,

Watishie pasipo soni,

Wakiuke kwa matarajio,

Kwamba watadumu siku zote.

 

Amka enyi mlio wa CCM,

Mapinduzi ya haki myaibue,

Hasira zenu ziwaondoe wasioistahili jamii.

Watoke, watoke kabla hamjatoka.

 

Msibwete enyi wana wa CCM,

Mkayaona mabaya na kuyaacha,

Kwa vile yanatendwa na wenye majina,

Mkashindwa kuwakemea, kuwatimua.

 

Mtayaonja mauti ya kisiasa,

Kwa uzembe wa wasio haki,

Wakitisha na kukiuka,

Ubunge wenu mkavuliwa.

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO