Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Father Festus: WANAUME WASINDIKIZENI WAKE ZENU KILINIKI


Festus Makwame wa Kanisa la Katoliki Sent Treza Jimbo la Arusha akiwa anafurahiajambo wakati akiwa anaendesha ibadaya mkesha wa sikukuu ya christimas hapo jana usiku Jijini Arusha.Picha naVero Ignatus Blog.
Baadhi ya waumini waliohudhuria katika ibada hiyo ya mkesha wa sikukuu ya Christmass ni pamoja na maharusi hawa .Picha na Vero Ignatus Blog
             Father Festus Makwame akiwa amembeba mafano wa mtoto Yesu aliyezaliwa ilipotimia majira ya saa sita kamili za usiku katika kanisa la Katoliki Sent Treza Jimbo la Arusha .Picha na Vero Ignatus Blog.
fFather Festus Makwame akiwa anahubiri katika mkesha wa sikukuu ya christimasiliyofanyika katika kanisa la Katoliki Sent Treza Jimbo laArusha.






Maharusi Denis na bi Joviety wakiwa ibadani muda mfupi kabla ya kufunggishwa ndoa kanisani hapo.Picha na Vero Igantus Blog

Maharusi hawa bwana Charles na bi Sabilina waliweza kufunga ndoa katika mkesha huo wa sikukuu ya christma katika kanisa la Katoliki Sent Treza Jimbo la Arusha .Picha na Vero Ignatus Blog.


Na,Vero Ignatus.Arusha.

Wito umetolewa kwa wanaume kuwa makini na kuwasindikiza wake zao kiliniki wakati wakiwa wajawazito kwani yapo mambo muhimu watakayojifunza wakiwa pamoja yatakayomsaidia mama na mtoto kuwa salama hadi wakati wa kujifungua.

Hayo yamesemwa na father Festus Makwame wa kanisa katoliki Sent Treza jimbo la Arusha alipokuwa kwenye ibada ya mkesha wa sikukuu ya krismas na kusema kuwa wanaume wengi hawana tabia ya kuwa na wake zao pindi wanapokuwa wajawazito jambo ambalo ni kosa kubwa

“Wanaume wasindikizeni wake zenu kiliniki huoni kwamba anashirikiana na Mungu katika uumbaji tena anakujengea heshima yawewe kuitwa baba Fulani?nenda nae yapo mambo mengi mtakayoelekezwa hata namna ya vyakula anavyotakiwa kula akisahau kwa vile ulikuwepo utamkumbusha?hebu igeni mfano wa Joseph na Maria hadi Yesu Kristo anazaliwa walikuwa pamoja.”alisisitiza

Amewataka waumini waliohudhuria ibada hiyo ya mkesha wa christmas waamue kubadilika waruhusu Kristo azaliwe mioyoni mwao ili mambo yao yawe mapya ,huku akisisitiza msamaha wa kweli pale mmoja anapomkosea mwingine kwani ni jambo ambalo Mungu analifurahia

“Wacha tuwe wakweli hakuna jambo gumu kama kumsamehe mtu aliyekukosea tena kwa makusudi,lakini kwa vile Mungu ameagiza tusameheane ni lazima tufanye hivyo na ukweli utabakia kuwa hivi Msamaha wa kweli ni ule ambao unautoa huku Unauma umekosewa lakini unasamehe kwa faida yako mwenyewe pia.”Alisisitiza father Festus.

Aidha amesema kuwa katika ibada hiyo ya mkesha wa krismas amewataka waumini kuachana mila na desturi potofu ambazo hazimpendezi Mungu kwani ni uvuli wa mauti.

“Wacheni michanganyo michanganyo kwani haimpendezi Mungu jamani kama umeamua kuwa kwa Mungu ,basi mfuate ili upate uzima wa milele ,na kama mwenzetu umeamua kumfuata shetani basi mfuate uangamie kwaani mambo haya ya michanganyiko michanganyiko mkiiendekeza huwa inaleta balaa na mikosi katika familia zenu”alisema father Festus.
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO