Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Lema Apata Ahueni, Apewa Siku 10 Kuwasilisha Rufaa Yake!

Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema akiteta jambo na mke wake Neema Lema Tarimo katika chumba cha Mahakama Kuu Kanda ya Arusha jana. Picha na Vero Ignatus Blog.

Arusha
  Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha Dkt.Modesta Opiyo  amempa siku kumi(10) Mbunge Godbless Lema kupitia mawakili wake wawe wamewasilisha notisi ya kukata rufaa dhidi ya maamuzi ya mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha iliyomnyima dhamana kwa kosa la uchochezi.

Agizo hilo limekuja kutokana na mahamama kutoridhishwa na hoja za maombi ya mapingamizi mawili yaliyowekwa na mawakili wa serikali dhidi ya taarifa ya dharura ya kusudio la kukataa rufaa ya mawakili wa mbunge huyo
Jaji  Dkt.Modesta Opiyo  wa Mahakama Kuu kanda ya Arusha alisema katika maamuzi yake kuwa pingamizi zilizowekwa hazina msingi kwani waleta maombi walifuata taratibu zote za katika kiapo na hati ya dharua ya kuitwa mahakamani, ambapo amesema mahakama haijaona ucheleweshwaji wa lazima.

Baada ya uamuzi huo Jaji Opiyo aliwataka mawakili wa Lema ,Shekh  Mfinanga na Faraji Mangula kuwasilisha notisi ndani ya siku kumi kuanzia jana, hadi hapo tar 30 Disemba 2016 shauri hilo litakaposikilizwa tena.
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO