Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Taarifa Kutoka BAVICHA Arusha: Mwaliko wa Kushiriki Uchangiaji Damu Hospitali ya Mt Meru Kesho Ijumaa Disemba 23, 2016

Makataba: Katibu wa BAVICHA Wialaya ya Arusha Mjini ambaye pia ni Diwani wa Viti MaalumKata ya Levolosi Mh Glory Kaaya (kushoto) akiwa pamojana Diwani wa Levolosi (CHADEMA) Mh DiwaniNanyarokatika moja ya vikao  vya chama hicho siku za nyuma. Picha na Mosec Joseph

Baraza la Vijana  wa CHADEMA (BAVICHA) Wilaya ya Arusha Mjini tutakua na event  ya kufunga Mwaka 2016 kwa kushiriki  kujitolea kuchangia Damu katika Hospital ya Mt.Meru siku ya ijumaa tarehe 23/12/2016 saa 3:00 asubuhi.

Baraza linawakaribisha vijana wote na wananchi wote  wa Jiji la Arusha kushiriki pamoja kusaidia wengine leo kwako kesho kwangu .

Tuungane pamoja kutoa mchango wa damu kwa ajili ya wenzentu wenye uhitaji!
Imetolewa na
Mh Glory Kaaya
(Diwani viti maalum)
Katibu BAVICHA (W).  0767533992
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO