Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Meya wa Jiji la Arusha Kalisti Lazaro Amtunuku Cheti cha Shukrani Diwani Wake kwa Msaada wa Taasisi yake kwa Jiji Kujenga Vyumba vya Madarasa 11 Olasiti

Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha Mh Kalisti Lazaro Bukhay akimpongeza na kumpatia cheti cha shukrani Mkurugenzi wa  kampuni ya Achieve in Africa Mh Alex Marti kwa kusaidia kufadhili  sare za shule kwa watoto 400 wanaoishi katika mazingira magumu, kusaidia ujenzi wa madarasa 11 na madawati 280 shule ya msingi Olasiti ambayo inasimamiwa na Halmashauri ya Jiji.

Achieve in Africa imesaidia pia upatikanaji wa madawati 60 na ujenzi wa matundu 20 ya choo kwa shule ya  sekondari Olasiti.

Mh Kalisti amempongeza mkurugenzi huyo ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Olasiti kupitia CHADEMA na kumkabidhi cheti kama tuzo maalumu katika ofisi ya Meya kwa niaba ya taasisi ya Achive in Africa kupongeza juhudi binafsi za diwani  huyo na taasisi hiyo kuisaidiana na Halmashauri ya Jiji kutatua changamoto zinazoikabili jamii ya Arusha nje na bajeti rasmi iliyotengwa na Halmashsuri.

Baadhi ya majengo ya madarasa na vyoo yanaendelea  kumaliziwa ujenzi wake na na  Halmashauri ya Jiji la Arusha.
Diwani wa Kata ya Olasiti Jijini Arusha kupitia CHADEMA, Mh Alex Mart (kulia) akipokea cheti cha shukrani kutoka kwa Meya wa Jiji la Arusha ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Sokoni I, Mh Kalisti Lazaro Bukhay
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO