Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Mbunge wa Rombo Joseph Selasini Kusherehekea Mwaka Mpya Kwa Kupanda Miti na Wananchi Wake

Mbunge wa Rombo Mh Joseph Selasini (CHADEMA) ataongoza mamia  ya vijana na wanajamii wengine katika uzinduzi wa kampeni ya upandaji miti jimboni humo  kesho January 1, 2017 katika eneo la Mamsera.

Zaidi ya miche  1000 ya miti imeandaliwa kuoteshwa maeneo mbalimbali ya Jimbo  la Rombo katika jitihada za kukabiliana na uharibifu wa mazingira kutokana na ukame uliotokana na tabia ya wananchi kukata miti bila kuotesha miti mbafala.

Zoezi hilo  linatarajiwa kuhitimishwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mh Agnes Hokororo eneo la Mkuu yalipo makao  makuu  ya kiutawala ya Wilaya ya Rombo.


Picha ya Maktaba: Mbunge wa Rombo Mh Joseph Selasini akikagua athari za mvua mwaka jana kati Wilaya yake ya Rombo.
Picha: www.brotherdanny.com
Wilaya ya Rombo ambayo kijiografia ndiko ulipo mlima Kilimanjaro imeathirika sana na mabadiliko ya tabia nchi kiasi cha kufikia kukauka kwa vijito na chemchemi nyingi na kupelekea adha kubwa ya upatikanaji maji tofauti na zamani.

Wenyeji wameiekeza blogu hii kuwa joto limeongezeka sana na mvua hazitabiriki tena huku theluji mlimani ambayo husababishwa na unyevu nyevu wa miti kwenda mlimani inayeyuka.
Mh Mbunge anawakaribisha watu wote kushiriki kampeni hii muhimu kwa ajili ya vizazi vya sasa na vijavyo
Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO