Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

James Ole Millya Avuna Magamba 70 Magadirisho–Usa River, Arumeru jana

SAM_3832

James Ole Millya akilakiwa na wananchi wakati anawasili eneo la mkutano, jirani na ofisi ya CCM ya Kijiji cha Magadirisho kilichopo eneo la Usa-River Wilayani Arumeru.

SAM_3829Katibu wa Mbunge wa Arumeru Mashariki, Ndg Toti Ndone, ambae pia ni Katibu wa Cama Wilaya, akifafanua masuala mbali mbali ya kiutendaji na kuainisha juhudi za Mbunge huyo kijana zilizofanyika hadi sasa katika kushugulikia maswala ya ardhi, maji, na swala la ajira kwa vijna na kina mama na aadi nyingine alizozitoa wakati wa kampeni. Ndondi alisema Usajili wa Shirika la Maendelo la Jimbo umekamilika na kwamba mwakani litaanza kusomesha watoto waishio kwenye mazingira magumu kiucumi. Pia akaelezea ziara ya Mbunge Nassari kwa Jimbo zima kuanzia mwezi ujao.

Kwa mujibu wa maelezo ya Katibu huyo, Nassari leo atakagua mradi wa maji eneo la Ngarenanyuki

SAM_3850James Millya akizungumza mkutanoni hapo ambapo pamoja na mambo mengine aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika zoezi la uboreshaji daftari la wapiga kura na kujiandikisha ili waweze kushiriki uchaguzi ujao na kuitoa CCM madarakani kwasababu imesindwa kubadili maisa yao. Alitoa wito pia kwa wananchi hao kushiriki mchakato wa katiba mpya na sensa ya watu na makazi kwa ukamilifu kwasababu ndio dira ya maendeleo.

Akikumbushia kilichomtoa CCM, huku akishangiliwa sana, alisema kuwa awezi kuwa seemu ya watu wasio na damira ya kuwakomboa watanzania kutoka kwenye lindi la umasikini uliokithiri. Akisisitiza zaidi alisema nchi imegeuzwa kuwa ya watu nane tu wanoitafuna kama watakavyo na kuahidi kuwataja majina siku nyingine.

Alisema tofauti anayoiona Chadema tofauti na alipokuwa CCM ni kuwa watu wa CHADEMA wanaupendo sana kwa kila mmoja.

Millya akizungumzia tatizo la ajira kwa vijna alisema vijana hawana matumaini na maisha na ambao wana matumaini ni wale ambao wazazi wao wana madaraka ccm au serikalini. Alitumia nafasi hiyo pia kuponda uteuzi wa MaDC na kulalamika kuwa hakuna hata mzawa mmoja kutoka Arusha alieteuliwa katika uteuzi wa hivi karibuni uliofanywa na Rais Kikwete.

SAM_3852 Millya akidondosha kadi za CCM zilizorudishwa

SAM_3881

Kadi zinakusanywa kwenye kilemba kilicosalimishwa pia

SAM_3882

SAM_3858Hapa Millya akigawa kadi kwa wanachama wapya

SAM_3888Millya akipita kukusanya michango ya wananchi kusaidia kazi za chama Waliayani humo, hususani kijijini hapo Magadirisho. Jumla ya Sh 195,550 zilipatikana

SAM_3830Wengine wakichangia kwa njia za mitandao

SAM_3899Makamanda wa chama hicho kutoka Arusha mjini wakishangaa namna ya utumaji michango kwa njia ya mitandao jinsi inavyofanya kazi

SAM_3866

SAM_3865

Millya akipokea wanachama wapya jukwaani

SAM_3837Watu wa bodaboda wakaweka kambi mbele ya Ofisi ya CCM ya kijijini hapo

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO