Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Wakazi wa Arusha waanza kuonja adha ya foleni barabarani

Katika miji mikubwa duniani swala la msongamano wa magari barabarani (traffic jam) ni la kawaida. Kwa mataifa yaliyoendelea wamejaribu kubuni mbinu mbalimbali za kukabiliana na adha ya foleni.

Hapa kwentu Tanzania, hususani kwa jiji la Dar es Salaam, foleni za barabarani zimekuwa kero kubwa kwa wananchi wengi na watafiti wameweza kuthibitisha kuwepo kwa athari kubwa sana kiuchumi kwa nchi.

Kwa muda mrefu imezoeleka kuwa Dar es Slaama ndio mahali ambapo wakaazi wake wanakosa raha ukifika muda wa kurudi kutoka makazini. Lakini sasa baadhi ya miji mingine nayo inaonekana kukumbwa na kadhia hiyo.

Wakazi wa Jiji la Arusha wameanza kuona kero ya foleni za magari barabarani tofauti na hapo awali. Hali imekuwa ya msongamano zaidi hasa kipindi hiki ambacho kuna ukarabati mkubwa unaendelea mjini hapa wa kuboresha barabara zote kuu za mjini kwa kiwango cha lami. Unafuu pekee unaoonekana ni vile foleni ya Arusha inasogea tofauti na Dar ambako kuna wakati dereva anakwama mahali kiasi cha kulazimika kuzima gari yake kabisa.

SAM_3508Picha hii inaonesha hali halisi ya msongamano barabarani kwa maeneo mengi ya jiji la Arusha hivi sasa.

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO