Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

More Updates Mlipuko Arusha: Simulizi za Jinsi Mlipuko Ulivyotokea na Jinsi Mshukiwa Alivyokamatwa! Angalia picha za majeruhi hapa…

Leo asubuhi mlipuko wa mabomu uliotokea katika kanisa la kikatoliki la Mt Joseph Mfanyakazi – Olasiti Jijini Arusha. nakupelekea vifo na majeruhi kwa baadhi ya waumini waliohudhuria katika sherehe ya uzinduzi wa Parokia katika kanisa hilo, mgeni rasmi akiwa Balozi wa Papa wa Vatican.

Blog hii iliendelea kufuatilia tukio zima na hii ni ripoti ya hadi jioni ya leo…

Chanzo

Kijana huyo(chini pichani aliyevalia tisheti ya njano) ameeleza kwamba bomu hilo lilirushwa na kijana mmoja ambaye kimwonekano alikuwa ni kijana wa kati ya miaka 20-25, na kwamba baada ya kijana huyo kurusha bomu alikimbia kutoka eneo hilo.

Kukamatwa kwa mtuhumiwa

Kuna kijana ambaye alishirikiana na wananchi wengine kumkimbiza mtuhumiwa kutoka Olasiti mlipuko ulipotokea hadi katika kijiji kiitwacho Ndorobo.

Kijana huyo (mtizame mwisho kabisa katika post hii) alisimulia kuwa mtuhumiwa alikimbia kisha alijilaza katika miwa asionekane ila kwa msaada wa mbwa waliokuwa wakimkimbiza mtuhumiwa huyo walifanikiwa kumkamata na mara baada ya kumkamata walimkuta akiwa na mfuko wenye mabomu yalizobakia.

Muda mfupi baadae wananchi wenye hasira kali walifika eneo alipokamatiwa mtuhumiwa huyo wakiwa na silaha kali za jadi wakitaka kumuua kijana huyo lakini Polisi waliokuwa wakisaidiana na wananchi hao walifika eneo lile nakumchukua mtuhumiwa huyo.

Waliojeruhiwa ni pamoja na Consensia Mbaga(53) Christopher Raymond (10),Deborah Joachim(24) Elizabeth Isdori(24),Anna Didas(52), Bertha Cosinery(49),Edda Ndowo(77) Derick Cyprian(8),Faustine Andrea (35),Mary okech,Neema Daud(13).
Watu wengine ni Mesoit Siriri (33) ,Clenes pius(22),Joyce yohana (15) ,Restuta Alex(50), Mathias Riha (74), Magreth Andrew(45), James Gabriel (16), Regina James (17), Elizabeth Masawe(15), Elizabeth Sauli(18), Njau (35),Yasinta Msafiri (160 na Doreen
Pancras(28). Idadi wajeruhi wengine ni Alex Arnold,Agripina Alex(9),James
Gabriel(16),loveness nelson (17) ,Amalone Pius(25),Frank Donatus (10) ,Alphonce Nyalandu (26),Athanasia Reginald (14),Phillemon Ceressa(49) ,Neema Daud(13)Sophia Kanda(72) ,Theofrida Inocent(21), na Regina Darnes(17).

Hatujaweza kupata jina la mwanakwaya aliyefariki na mtuhumiwa aliyekamatwa kwa sasa…

Dakika chache baada ya mlipuko hivi ndivyo watu walivyodhurika

 wananchi wakiwa wameanguka chini huku wengine wakiwa wanakimbia mara baada ya mlipuko kutokea katika kanisa la mtakatifu joseph

 hapa maaskofu na balozi wakiwa wanabariki chumvi kabla ya mlipuko kutokea hivi leo

maafisa polisi wakiwa wanachunguza ni bomu la aina gani limetupwa hapo

mmoja wa majeruhi akipatiwa huduma

sehemu bomu lilipotua

Baadhi ya wananhi waliofika hospitali ya Mt Merru

Kijana aliyeeleza kushuhudia mlipuko ulivyotokea akisimulia hali ilivyokuwa

Tunaomba radhi kwa picha hii! Mmoja wa waliofariki, alikuwa mwanakwaya

Kijana aliyemkimbiza mtuhumiwa akisimuliza jinsi alivyoweza kumkimbiza mtuhumiwa hadi kumkamata.

Jengo la Kanisa Jipya lililokuwa lizinduliwe leo

Askari wakilinda usalama kwenye eneo la tukio Olasiti

Mabaki ya viatu huku Polisi wakianza kuchunguza mlipuko

Padri na Mtawa ambao hawakufahamika majina yao mara moja wakiwa hawaamini kilichotokea

Balozi wa Vatican nchini,Askofu Mkuu Fransis akiondolewa kwenye eneo la Kanisa hilo kwa usalama wake

Balozi wa Vatican hapa nchini,Askofu Mkuu Fransis akiingia kwenye gari kuondoka

Majeruhi

majeruhi mwingine

Mtoto nae alikuwa miongoni mwa walioathirika

Majeruhi alionekana kusaidiwa muda wote

Mama huyu akiugulia maumivu

Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha,Liberatus Sabas akizungumza na waandishi wa habari kuwa mtuhumiwa mmoja anashikiliwa kwa mahojiano kufuatia tukio hilo

Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Magesa Mulongo akizungumzia tukio hilo na hatua za kusaidia majeruhi

Mbunge wa Arusha Mjini,Godbless Lema na Mbunge wa Arumeru Mashariki wakiwasili eneo la tukio Olasiti

Padri Festus Mangwangi

Wananchi waliojitokeza kushuhudia

Mbunge wa Arumeru Mashariki,Joshua Nassari(kushoto)na Mbunge wa Arusha Mjini,Godbless Lema wakimfariji majeruhi

Credit: Nyumba ya Habari na Filbert Rweyemamu

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO