Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

TASWIRA MAHAKAMANI IRINGA: MBUNGE MSIGWA NA WENZAKE WAACHIWA KWA DHAMANA 27 WAKOSA DHAMANA KESI KUTAJWA TENA 3 MWEZI WA 6

 


Wafuasi  wa Chadema Iringa  wakiwa  wamembeba  juu juu mbunge  wa  jimbo  la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa  baada ya  kuachiwa kwa  dhamana  leo hadi kesi  hiyo itakapotajwa tena Juni 3 mwaka  huu  huku wafuasi  wake  26 kati ya 74 wakosa  sifa  ya  dhamana

Mbunge  Msigwa akishuka katika gari ya  polisi huku akiwa chini ya ulinzi mkali  wa  FFU leo  alipofikishwa mahakamani kabla ya  kudhaminiwa

Mheshimiwa mbunge  Msigwa  akishuka katika gari ya  polisi chini ya ulinzi mkali  wa polisi

Mkuu  wa FFU Iringa Said Abdalah Mnunka  (katikati) akiwa na maofisa  wenzake  wa  polisi

Katibu  wa Chadema wilaya ya Iringa mjini Bi Suzana Mgonakulia  akitoa nje ya mahakama hiyo

mbunge Msigwa akiwa amebebwa  juu juu na  wafuasi  wa Chadema jioni  hii

SAKATA la vurugu  za machinga na polisi mjini Iringa limechukua  sura  mpya  baada  ya  jeshi la  polisi mkoa wa Iringa  kumfikisha mahakamani mbunge  wa jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa pamoja na  watuhumiwa wengine zaidi ya 70

Huku mahakama   hiyo  ikitoa masharti nafuu ya dhamana kwa  watuhumiwa hao na  kuwaonya  kutofanya  kosa kwa  kipindi  chote  cha kesi  hiyo inapoendelea  kusikilizwa .

Watuhumiwa hao  walifikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi wa wilaya ya Iringa Mheshimiwa Godfrey Isaya  leo  majira ya saa 8 mchana  huku wakiwa  chini ya ulinzi mkali  wa askari  wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) waliokuwa na msafara  wa magari zaidi ya matatu  likiwemo  gari ya maji ya  kuwasha .

Mbali ya mbunge Msigwa  kupanda gari ndogo  ya  wazi ya  polisi pamoja na  watuhumiwa  wawili wanawake  waliokamatwa katika  vurugu  hizo bado  watuhumiwa  wengine 74  walitumia usafiri wa karandinga la polisi .

Mbele  ya mahakama  hiyo  wakili  wa serikali  Adolph Maganda alisema  kuwa  watuhumiwa hao kwa pamoja  wanatuhumiwa  kwa kosa kwa makosa matatu  likiwemo la kufanya kushiriki  mkutano na kufanya   vurugu ,uchechezi na kuharibu mali kinyume na sheria 

Huku mbunge  akisomewa mashitaka mawili likiwemo  kushawishi   na kufanya mkutano bila  kibali  .
Watuhumiwa  wote  wamekana  mashitaka  dhidi yao  huku  wakili  wa  serikali akidai  kuwa hana pingamizi na dhamana kwa  watuhumiwa hao wote  hata  hivyo wote   wamekana  mashitaka  yote yaliyotolewa  dhidi  yao .

Hata  hivyo makimu anayesikiliza kesi  hiyo alisema kuwa dhamana kwa  washitakiwa  wote  ipo  wazi  kwa kila mmoja kuwa mdhamini mmoja anayeaminika pamoja na kusaini hati ya dhamana  ya Tsh milioni moja .

Hadi majira ya  saa 10 jioni mahakama  hiyo  ilikuwa ikiendelea na mchakato  wa  kupitia barua  za dhamana kwa  wadhamini  huku  mbunge akiwa  wa kwanza kudhaminiwa ,mbali ya  mbunge  watuhumiwa kati ya 74  waliokuwa  bado kupata  wadhamnini  ni  watuhumiwa  sita pekee.

Katibu  wa chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) wilaya ya Iringa mjini Suzana Mgonakulima alisema  kuwa  mchakato  wa  kuwadhamini  watuhumiwa  wote  waliosalia unaendelea kufanyika na kuwa wana uhakika wa  watuhumiwa  wote kudhaminiwa .

Hadi  majira  haya  ya saa 10 .40  mbunge  msigwa na  wengine  wameachiwa  huku  watuhumiwa 26 kati ya 74  wamekosa  dhamana hadi kesi hiyo itakapotajwa  tena tarehe 3 /6/2012

Wakati  huo  huo  wananachi  waliofika  mahakamani hapo  kushuhudia mbunge  wao akifikishwa mahakamani  wamempongeza mkuu  wa  kikosi cha kutuliza ghasia mkoa  wa Iringa (FFU) Said Abdulah Mnunka  kwa kusimamia amani na utulivu katika  eneo hilo la mahakama na jinsi ambavyo alivyoweza  kupambana na machinga  pasipo kumwaga damu kwa  siku ya  jana wakati  wa vurugu  hizo

MATUKIO ZAIDI

Watuhumiwa  6 kati ya  74  waliofikishwa mahakamani kutokana na vurugu za machinga na polisi bado  kudhaminiwa  na mchakato  wa kuwadhamini  unaendelea  kufanyika  hadi  sasa na  wana Chadema  wanaendesha mchango mahakamani ili  kupata  pesa ya  kupiga  picha  kwa ajili ya kuwashughulikia  dhamana

Askari  wa FFU  wakiendelea  kulinda  eneo la mahakama ya  wilaya ya Iringa  jioni ya leo  huku watuhumiwa  wakiwa bado kutoka mahakamani

Ulinzi  mkali kweli kweli

Karani  wa mahakama  Bi , Grace  akiita majina ya  wadhamini mahakamani hapo

CHANZO: HTTP://MATUKIODAIMA.COM

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO