Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Sherehe ya Lady Jaydee kuadhimisha Miaka 13 katika Muziki Imeahirishwa kupisha Msiba wa Albert Mangwea “Cow Boy” aliyefariki Afrika Kusini jana

0_f4c89Mwanamuziki nguli wa muziki wa kizazi kipya nchini, mwanadada Judith Wambura maarufu kama Lady Jaydee ‘Anaconda’ ametangaza kuahirisha shughuli ya maadhimisho ya miaka 13 tangu aanze muziki iliyokuwa imapangwa kufanyika Ijumaa hii ya Mei 31, 2013 katika mgahawa wake wa Nyumbani Lounge kupisha msiba wa kifo cha msanii Albert Robert Mangweha aliyeripotiwa kufariki nchini Afrika Kusini jana.

Judith amesema hayo muda mfupi uliopita (saa 3:52 asubuhi) wakati akihojiwa katika kipindi cha Super Mix ya East Africa Radio na mtangazaji Zembwela.

Jaydee ameeeleza uamuzi wake wa kutitisha show hiyo kuwa unalenga kutoa nafasi kwa wafiwa wote na wadau wa tansnia ya muziki na wapenzi wa Mangwea kumaliza taratibu za kumsitiri kipenzi chao na kueleza kwamba tarehe nyingine ya shughuli hiyo itatangazwa baadae.

Tangu amekaribishwa studio, Judith Wambura alionekana kuwa na majonsi sana kiasi cha kushindwa kuongea mara kwa mara na kukatisha mazungumzo yake kutokana na kukabwa na kilio.

Sherehe ya miaka 13 ya Lady Jay Dee katika muziki ilipangwa kuambatana na uzinduzi wa album yake ya sita inayo kwenda kwa jina la NOTHING BUT THE TRUTH ambayo ina jumla ya nyimbo 10, na  pia kungekuwa na show ya nyimbo zote bora za JayDee nikishirikiana na baadhi ya wasanii wenzangu hapa nchini.

Sherehe zitafanyika Ijumaa tarehe 31 May 2013.

lady jd  13yrsBango la matangazo ya sherehe hiyo ya Lady Jaydee iliyoahirishwa ambapo mdhamini mkuu kwa upande wa media ni East Africa TV.

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO