Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

WATUMISHI 10 WA JIJI LA ARUSHA WAPANDISHWA KIZIMBANI KWA KUJIPATIA MAMILIONI YA KIFISADI

Aliyekuwa Afisa Elimu wa Manispaa ya Arusha (Sasa Jiji), Fatma Laizer akiingia katika viwanja vya mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Arusha akisubiri kupandishwa mahakamani akituhumiwa kujipatia mamilioni ya fedha kupitia mishahara ya watumishi hewa pindi akiwa Afisa elimu.

Mmoja wa watumishi wa idara ya Afsa wakati ikiitwa Manispaa ya Arusha(sasa jiji), ambae jina lake halikupatikana akiingia kwenye viwanja vya mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Arusha akisubiri kupandishwa kizimbani kwa tuhuma za kujipatia mamilioni ya fedha kupitia mishahara hewa ya watumishi. kushoto ni Afisa mwingine wa Manispaa hiyo

Mmoja wa Maofisa wa Manispaa ya Arusha akiteremka kutoka kwenye gari la TAKUKURU kuelekea kwenye viwanja vya mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Arusha akisubiri kusomewa mashitaka kuhusu kujipatia mamilioni ya fedha kupitia mishahara ya watumishi hewa. hata hivyo walishindwa kupandishwa kizimbani leo kufuatia hati iliyowasilishwa mahakamani hapo kuonekana kuwa na makosa ya kisheria

Ofisa wa takukuru akimsubiri mmoja wa watuhumiwa wa kujipatia mamilioni ya fedha kupitia mishahara ya watumishi hewa akiwa mtumishi katika manispaa ya Arusha baada ya kumfikisha mahakamani hapo

Mmoja wa watuhumiwa akiingia mahakamani hapo baada ya kuteremka kutoka kwenye gari la Takukuru

Published  by Pamela Mollel on May 16, 2013

Washirikishe Google Plus

About Unknown

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO