Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe Amtembelea Balozi wa Vatican na Mwakilishi wa Papa Nchini Tanzania Francisco Montecillo Padilla na kumpa pole

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akisalimiana na Mhe. Francisco Montecillo Padilla, Balozi wa Vatican na Mwakilishi wa Papa hapa nchini mara baada ya kuwasili Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumsalimia na kumpa pole kufuatia shambulio la bomu  lililotokea Jijini Arusha tarehe 5 Mei, 2013  na kupelekea watu watatu kufariki dunia na wengine zaidi ya 60 kujeruhiwa. Balozi Padilla alikuwa miongoni mwa wageni waalikwa  katika hafla ya ufunguzi rasmi wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasiti, Jimbo Kuu la Arusha wakati tukio hilo linatokea.

Mhe. Balozi Padilla akiwa katika  mazungumzo na Mhe. Membe kuhusu tukio hilo  ambapo pamoja na mambo mengine alisema kuwa anaamini suala hilo litapita na wahusika kupatikana na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Mhe. Membe akiagana na Mhe. Balozi Padilla mara baada ya kuzungumza naye.Picha na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO