Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

TASWIRA: MAZISHI YA WATU WALIOLIPULIWA NA BOMU KANISANI ARUSHA

Maaskofu wakiombea miili ya marehemu Regina Loning'o Laizer ,James Gabriel Kessy na patricia Assey  kabla ya kuingizwa kanisani tayari kwa ibada ya mazishi iliyofanyika katika kanisa la mtakatifu josephy mfanyakazi lililopo katika kata ya olasiti mjini hapa ambapo marehemu hawa ambao walifariki dunia may 5 wakati wakisali katika ibada ya uzinduzi wa kanisa ambapo mtu asiyejulikana alirusha bomu wamezikwa nje ya kanisa hilo. Picha hii imepigwa na Woinde Shizza

Majeneza yakiwa kanisani kabla ya ibada ya mazishi

Mapadri wakiwa wamebeba moja ya majeneza

Watawa wakiwa kanisani wakati wa ibada

Viongozi wa Kanisa wakitoa salamu za mwisho

Kilio kilio kilio anamlilia mama yake mzazi

Wananchi wakitoa salamu zao za mwisho kwenye kanisa katoliki

Majonzi na uchungu

Wahudumu wakishusha mwili wa marehemu kaburini kwenye viwanja vya Kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Parokia ya Olasiti jijini Arusha

Wahudumu wakishusha mwili wa marehemu kaburini kwenye viwanja vya Kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Parokia ya Olasiti jijini Arusha

Baadhi ya maaskofu kutoka majimbo mbalimbali waliohudhuria ibada ya mazishi leo

Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheri Tanzania(KKKT)Dk Alex Malasusa(kushoto)akiwa na viongozi wengine wa Kanis a hilo wakiwa kwenye ibada ya mazishi

Umati wa watu waliohudhuria maziko hayo

Waziri Mkuu mstaafu,Edward Lowassa(kulia)akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Ndani,Dk Emmanuel Nchimbi kabla ya ibada kuanza. Kuanzia picha ya pili: Filbert Rweyemamu

Waziri wa Mambo ya ndani, Dk Emmanuel Nchimbi akiweka shada la maua kwa niaba ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aliyeondoka kabla ya zoezi hilo kufanyika, katika ibada ya mazishi  ya waumini waliokufa baada ya kulipuliwa na blomu katika Kanisa la Katoliki la Mt Josephat Mfanyakazi – Parokia ya Olasiti, Arusha.

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa akitoa heshima za mwisho kwa moja ya miili hiyo.

Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, Freeman Mbowe akiweka shada la maua katika moja ya makaburi hayo.

Majeneza yenye miili ya marehemu ikiwa kanisani tayari kuombewa. Marehemu hawa walifariki katika mlipuko wa bomu katika Kanisa la Mt Josephat Mfanyakazi – Parokia ya Olasiti, Arusha wakati ibada ikiwa ineendelea.

PICHA NA SEIF MANGWANGI, FILBERT RWEYEMAMU NA WOINDE SHIZZA

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO