Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Multichoice Tanzania yajikita katika kusambaza Digitali katika shule za msingi Tanzania.

Meneja Uhusiano wa MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi akiwakaribisha wageni wanahabari katika hafla mchapalo ya kusheherekea Africa Day na Dstv ambapo amesema DStv inatoa nafasi kwa wateja wake kuwa na fursa ya kuchagua vifurushi mbalimbali kulingana na uwezo wa mteja ambacho cha uwezo wa chini kabisa ni Access chenye zaidi ya channeli 40 gharama yake ni nafuu sana ambapo mteja atalipia shilingi 16,500 kwa mwezi. (Picha na Zainul Mzige wa dewjiblog).

Meneja wa Fedha wa kampuni ya Multichoice Tanzania, Bw. Francis Senguji akizungumzia malengo ya DStv Tanzania ambapo amesema wao kama waendeshaji wa biashara nyingine barani Afrika wanaojali na kuthamini maendeleo ya jamii wameona ni wajibu kusaidia jamii ili kuweza kuendeleza maendeleo ya kijamii nchini Tanzania.

Kwa kuendeleza hilo Multichoice ina mfumo wa kutoa elimu mashuleni ( Multichoice Resource Centre) hivyo watamumia jukwaa la Teknolojia kama darasa kwa njia mbalimbali kuwapa jamii nafasi ya kuendeleza vipaji na ujuzi.

Mfumo huo kutoa rasilimali kwenye shule kama vile ving'amuzi vya Satellite, VCRs/DVD na kifurushi cha elimu cha Dstv. Mpaka sasa Multichoice imeanzisha vituo vya rasilimali jamii katika shule 82 nchi nzima kwenye mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Iringa, Kagera, Mbeya, Pwani na Tanga.

Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo (katikati) akifafanua jambo wakati wa hafla mchapalo katika kusheherekea usiku wa Africa Day na DStv. Kulia ni Meneja Masoko wa Kampuni hiyo Furaha Samalu na kushoto ni Meneja Uhusiano wa Kampuni hiyo Barbara Kambogi.

Waalikwa katika hafla mchapalo ya kusheherekea usiku wa Africa Day na DStv katika Hoteli ya New Africa ya jijini Dar usiku wa kuamkia leo.

Kutoka kushoto ni Meneja Masoko wa Multichoice Tanzania Furaha Samalu, Blogger John Bukuku wa Fullshangwe Blog, Meneja Uendeshaji wa kampuni hiyo Ronald Shelukindo, Mdau wa DStv na Meneja wa Fedha katika kampuni hiyo Bw. Francis Senguji wakipozi kwa picha.

Meneja Uhusiano wa MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi (kulia) akifurahi jambo Wanahabari Sidi Mgumia (katikati) na Mama Mhina.

Ronald Shelukindo na Mdau LEMUTUZ wa Blog ya jamii.

Kutoka kushoto ni Meneja Masoko wa Multichoice Tanzania Furaha Samalu, Meneja Uendeshaji wa kampuni hiyo Ronald Shelukindo, Meneja wa Fedha katika kampuni hiyo Bw. Francis Senguji na mdau wa DStv wakipozi mbele ya camera yetu wakati wa hafla ya kusheherekea African Day na DStv iliyowakutanisha waandishi wahabari kutoka vyombo mbalimbali nchini.

Bloggers wakishow love...Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Fullshangwe Blog John Bukuku, William Malecela wa Blog ya wananchi a.k.a LEMUTUZ na Operations Manager wa Mo Blog Zainul Mzige a.k.a Bigzee katika hafla mchapalo ya kusheherekea African Day na DStv katika Hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam.

Wanahabari wakiwa bize kujaza Quiz iliyotolewa na kampuni ya Multichoice Tanzania ambapo mshindi kwanza amezawadiwa Full Set ya King'amuzi cha Dstv na 'Subscription' ya mwezi mmoja na washindi kumi wamezawadiwa kofia na T-shirts za Supersport moja ya chaneli zinazopatikana katika king'amuzi cha Dstv.

Wanahabari wakiendelea kuumiza kichwa huku wengine waki-google majibu ya Quiz hiyo kupitia simu zao za kiganjani.

Mtangazaji wa Radio Dennis Buslwa a.k.a Ssebo (kulia) akiwa busy kutafuta majibu ambapo tunahisi alikwa anawasiliana na watu wa Mo Blog wampe majibu kamili. Wengine ni Kamera Man wa Channel Ten na Mtangazaji wa Radio Salma Msangi pamoja na mdau wa Star Tv.

Barbara Kambogi akiteta jambo na Angela Msangi wa TBC.

Dada Revina Bandihai wa kampuni ya Multichoice Tanzania na HR Manager wa kampuni hiyo.

Ronald Shelukindo na Dada Furaha Samalu wakifungua mziki wa Kiafrika huku Bw. Francis Senguji akiserebuka na mdau.

Mkurugenzi wa Fullshangwe Blog John Bukuku akiserebuka na Meneja Uhusiano wa Multichoice Tanzania Barbara Kambogi wakati wa hafla hiyo.

Salma Msangi akionekana Kiafrika zaidi akiyarudi na Khadija Kalili wa Jambo leo.

Kwaito ilichezeka kisawa sawa....Chezea Multichoice wewe.....Ilinogaje.!

Kutoka kushoto ni Blogger Cathbert Angelo wa kajunason Blog, Mpiganaji Fadhili Akida na Blogger Othman Michuzi wa mtaa kwa mtaa Blog wakipoowz mbele ya kamera yetu.

Bloggers katika picha ya pamoja.

Dada Revina Bandihai wa Multichoice Tanzania na Bw. Francis Senguji wakisataka Rhumba wakati wa hafla hiyo.

Meneja wa Fedha wa Multichoice Tanzanua Bw. Francis Senguji akimpongeza Ssebo baada ya kuibuka mshindi katika Quiz iliyoendesha na Kampuni hiyo ambapo alinyakua Full Set ya King'amuzi cha Dstv na 'Subscription' ya mwezi mmoja.

Pichani juu na chini Meneja Uhusiano wa Multichoice Tanzania Barbara Kambogi akigawa Kofia na T-shirts kwa washindi wa Quiz ilyoendeshwa na kampuni hiyo wakati wa kusheherekea Africa Day na Dstv.

Dada Revina Bandihai (kushoto) wa Multichoice Tanzania akishow love na washindi wa Quiz iliyoendeshwa na kampuni hiyo.

Wanahabari wakishow love...Thank you DStv for the Cocktail Party to celebrate Africa Day with DStv.

CHANZO: HAKINGOWI.COM

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO