Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

TANGAZO KUTOKA CHUO CHA UHASIBU ARUSHA : CHUO KUFUNGULIWA ALHAMIS MEI 23, 2013

 

CHUO CHA UHASIBU ARUSHA

TAARIFA YA KUFUNGUA CHUO

Chuo cha Uhasibu Arusha kinawatangazia Wanafunzi wote wa kozi

za ngazi ya Cheti hadi Stashahada ya Uzamili kwamba chuo

kitafunguliwa siku ya Alhamisi tarehe 23 Mei, 2013.

Kuanzia tarehe 23 hadi tarehe 27 Mei, 2013 kutakuwa na zoezi la

usajili katika lango kuu la kuingia chuoni kwa kuzingatia masharti

yafuatayo:

1. Kila Mwanafunzi aliyeomba upya kujiunga na chuo anapaswa

kuonyesha kitambulisho chake cha chuo.

2. Kila Mwanafunzi aje na risiti au “Bank pay in slip” ya

kuonyesha malipo ya karo na fedha zote anazodaiwa na chuo.

3. Kila Mwanafunzi anapaswa kuingia mkataba mpya na Chuo.

Mkataba huo unapaswa kusainiwa kabla Mwanafunzi

hajasajiliwa.

4. ANGALIZO: Hakutakuwepo na usajili baada ya tarehe 27 Mei,

2013.

Mkuu wa Chuo

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO