Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Taswira: CHADEMA Wakiendesha mafunzo kwa wanachama wake 81 ambao wanatoka katika Majimbo 27 ya Uchaguzi katika Kanda ya Nyanda za Juu kusini, Jijini Mbeya jana

Chama Cha Demokrasia na Mendeleo (CHADEMA) kimeendesha mafunzo kwa wanachama wake 81 ambao wanatoka katika Majimbo 27 ya Uchaguzi katika Kanda ya Nyanda za Juu kusini Mafunzo yanayofanyika Katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden City ya Jijini Mbeya.

Mkurugenzi wa Mafunzo na Organaizesheni wa Chadema Taifa Singo Bensoni alisema Lengo la Mafunzo hayo ni kuhakikisha wanapata wakufunzi 30606 nchi nzima ambao watatawanyika katika kila kitongoji nchi nzima kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi na kuunda matawi ya Chama hicho ikiwa ni pamoja na kukifikishama hadi ngazi ya Chini.

Alisema mafunzo hayo yalianza kutolewa kwa kuchukua wakilishi watatu kila Jimbo la Uchaguzi ambao baada ya kumaliza watafanya mitihani na kufuzu kuwa wakufunzi wa chama na kuongeza kuwa mbinu itakayotumika ni kuendesha mafunzo ya chini kwa chini bila kuvaa sare za chama wa kutumia magari ya matangazo na vipaza sauti.

Aliongeza kuwa katika mafunzo hayo yanahusisha wawakilishi wawili kila kanda ambao waliungana na wanachama wengine 10 wa Kitaifa ambao jumla walikuwa 30 ambao baada ya kufuzu mafunzo walirudi kufundisha katika kanda zao ambapo katika Kanda ya Mbeya ina wanafunzi 81,Arusha 96, Mwanza 72 na Shinyanga 60 ambao wanawakilishwa na watu watatu kila Jimbo la Uchaguzi.

Aidha alisema mafunzo hayo yanatolewa kutokana na ufadhili wa watu wa Ujerumani na kwamba wakufunzi hao watapewa Miezi miwili kuhakikisha wameyafikia maeneo yote nchini na kufanikiwa kuwapa elimu wananchi wapatao 30 kwa Mtu mmoja na kuunda Msingi tayari kwa maandalizi ya Uchaguzi mkuu ujao.

Mkurugenzi wa Mafunzo na Organaizesheni wa Chadema Taifa Singo Bensoni alisema Lengo la Mafunzo hayo ni kuhakikisha wanapata wakufunzi 30606 nchi nzima ambao watatawanyika katika kila kitongoji nchi nzima kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi na kuunda matawi ya Chama hicho ikiwa ni pamoja na kukifikishama hadi ngazi ya Chini

CHANZO: MBEYA YETU BLOG

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO