Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MBIO ZA UCHAGUZI WA UDIWANI ARUSHA: MWENYEKITI CCM KATA YA THEMI ATIMKIA CUF

Pichani ni aliyekuwa mwenyekiti wa CCM kata ya Themi Petro Ndarivoi (Kulia) akirudisha kadi ya chama cha mapinduzi kwa mwenyekiti wa chama cha CUF halmashauri ya jiji la Arusha Hamza Mustaph kwenye makao makuu ya chama hicho jana jioni

Wakati kipenga cha uchaguzi wa udiwani kikitarajiwa kupilizwa wiki ijayo pichani ni mwenyekiti wa CUF halmashauri ya jiji la Arusha Hamza mustaph akimpatia kadi ya chama hicho Aliyekuwa mwenyekiti wa CCM kata ya Themi Petro Ndarivoi aliyejiunga na chama hicho jana jioni na kupewa fomu ya kugombea udiwani wa chama hicho kata ya Themi.

Mgombea udiwani kwa tiketi ya chama cha wananchi CUF kata ya Themi kwenye uchaguzi utakaoanza wiki ijayo Petro Ndarivoi akizungumza na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya CUF halmashauri ya jiji la Arusha jana jioni wakati aliporudisha rasmi kadi ya CCM na kuchukuwa kadi ya CUF mbele ya mgombea udiwani kwenye kata ya ELERAI John Bayo na mwenyekiti wa CUF wilaya ya Arusha Hamza Mustapha.Picha na Mahmoud Ahmad-Arusha

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO