Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

BARCELONA YASHEREHEKEA TAJI KWA KUIFUNGA ATLETICO MADRID 2-1

barca2 47012

Nyota wa zamani wa Arsenal, Cesc Fabregas na Alex Song wakishangilia kwenye chumba cha kubadilishia nguo cha Barcelona

barca1 d6d78

Wachezaji wa Barcelona wakishangilia taji la La Liga

barca 2f88c

Alexis Sanchez alifunga bao la ushindi baada ya Lionel Messi kutoka

barca3 758e9

Radamel Falcao akishangilia bao lake

PAMOJA na kwamba Lionel Messi alishindwa kucheza jana kutokana na kusumbuliwa na maumivu, lakini haikuzuia Barcelona kushinda 2-1 dhidi ya Atletico Madrid usiku wa jana na kushangilia taji la 22 la Ligi Kuu Hispania. 

Messi alianza katika mechi ya kwanza ndani ya raundi sita kwa sababu ya kusumbuliwa na maumivu ya nyama za paja la kulia, lakini akaondoka uwanjani dakika ya 68 Barcelona ikiwa nyuma kwa bao 1-0 lililofungwa na Radamel Falcao dakika ya 52 na Barca ikakamilisha wachezaji wote watatu wa kubadilisha. 

Hata hivyo, Alexis Sanchez akasawazisha dakika ya 72 na kiungo wa Atletico, Gabi Fernandez akajifunga dakika ya 80 hivyo kuamsha pati la ubingwa kwa Barcelona, wakiivua rasmi ubingwa Real Madrid. 

Mapema siku hiyo, Valencia ilijiongezea matumaini ya kucheza Ligi ya Mabingwa kwa ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Rayo Vallecano.

Roberto Soldado alifunga mabao mawili kabla ya mapumziko, wakati Andres Guardado na Nelson Valdez wakakamilisha karamu ya mabao kipindi cha pili.

Huo ulikuwa ushindi wa pili mfululizo wa 4-0 kwa Valencia  na unamaanisha timu ya Ernesto Valverde inaizidi kwa pointi moja Real Sociedad, ambayo leo itakuwa mwenyeji wa Granada.

Malaga na Sevilla zote zina nafasi ya kucheza michuano ya Ulaya baada ya sare ya bila kufungana uwanja wa La Rosaleda.

Stori na Picha kwa msaada wa Jackson Audiface Blog

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO