Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

CHADEMA kuwasha mto viwanja vya NMC Arusha leo

DSCN9964

Hawa ni baadhi ya wafuasi wa CHADEMA waliojitokeza katika viwanja hivyo Aprili 7 mwaka huu kusikiliza tamko la chama baada ya Mahakama Kuu kutengua matokeo yaliyompa Ubunge Mh Lema.

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinatarajia kufanya mkutano mkubwa wa hadhara katika viwanja vya NMC , Jijini Arusha.

Mkutano huo utahutubiwa na Mwenyekiti wa chama hicho ambae pia ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzania Bungeni, Mh Freeman Mbowe pamoja na aliekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Mh Godbless Lema ambae amekuwa akitumiwa na chama chake katika programmu yao mpya maarufu kama “Movement for Change” akizunguka nchi nzima kuhamasisha mabadiliko tangu Mahakama Kuu Kanand ya Arusha itengue ubunge wake Aprili 5 mwaka huu.

Pamoja na mambo mengine, mkutano huo utawatambulisha wanasiasa wapya waliohamia chama hicho.

Tangia jana habari za kuwako kwa mkutano huo zimekuwa gumzo miongoni mwa wananchi hali inayohisiwa kukusanya watu wengi kuliko mikutano iliyotangulia. Wasiwasi huu ndio ulipelekea watu wasiojulikana kupita na gari mitaani wakitangaza kuwa kutakuwa na vurugu na kwamba Lema ameandaa watu wakavamie maduka ya watu baada ya mkutano.

Blog hii inaamini Jeshi la Polisi liko makini na litawachukulia hatua wale wote watakaojihusisha na vitendo vya vurugu bila kujali ni nani amewaandaa.

Mkutano huwo utakuwa live kupitia blog hii na website ya Arusha Mambo www.arushamambo.com kuanzia saa saba mchana.

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO