Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

CHADEMA yatoa fursa za ajira wajasiriamali wadogo Arusha

DSCN0031

Mjasiriamali huyu ameweka kituo chake jirani na Soko Kuu Arusha. Bidhaa anazozalisha ni kama zinavyoonekana pichani

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinaelezwa kuwa na wafuasi wengi katika Mkoa wa Arusha na maeneo ya jirani kiasi cha kupelekea tafsiri kuwa eneo hilo ndio ngome yake zaidi hasa kwa kipindi cha sasa katika siasa za ushindani nchini.

Kwa mgeni anaetembelea Jiji la Arusha kwa mara ya kwanza ni wazi atakutana na watu wa jinsia na rika tofauti wakiwa wamevalia mavazi ama kuvipamba na vitambaa au kitu chochote chenye rangi nne za chama hicho.

Hali hii inaonekana kama utamaduni sasa maana haya hufanyika muda wote na sio wakati wa kampeni pekee. Kuna baadhi wenye magari na pikipiki nao wanayaremba kwa chochote chenye rangi za CHADEMA.

Jambo hili lililzaimu Blog hii kufanya uchunguzi mdogo na kugundua kuwapo kwa wajasiriamali wengi ambao wameamua kujiajiri kutengeneza bidhaa za aina mbalimbali zilizopambwa kwa rangi za bendera ya CHADEMA na kuziuza ili kuendesha maisha yao.

Bidhaa hizo ni pamoja na T-Shirts, Skafu, Kofia, Sweta, Stika za magari, Bangili, Hereni, Mikufu, na vifutia jasho kwa wachezaji kwa kuvaa mkononi ama kichwani.

Baadhi yao wamekiri kunufaika na kukubalika kwa chama hicho kwa watu wengi mjini hapa jambo ambalo linafanya wepesi kwa wao wajasiriamali kujipatia kipato kinachowasaidia kuendesha maisha na wengine wakadai wanfanya kama sehemu ya kukitangaza zaidi chama hicho.

DSCN0024 Hizi ni bidhaa mabazo tayari zimekamilika kwa ajili ya kuuzia wateja. Bei ni kuanzia Sh 500 hadi 15,000 kwa bidhaa moja

DSCN0034 Hapa ni kwa vijana wanaotengeneza bidhaa za urembo wa asili jirani Arusha City Park. Nao wameamua kutumia fursa iliyopo kujiongezea kipato

  Kamera yetu iliwansa vijana hawa wakikatiza mitaa ya Jiji na bidhaa zao kutafuta wateja.

DSCN0044 Huyu ni mjasiriamali mwingine anaenufaika na umaarufu wa CHADEMA mjini Arusha. Ofisi yake, japo sio rasmi sana ipo jirani na Msikiti wa Ijumaa mjini hapa.

DSCN0023 Kamera yetu pia ilimnasa kijana huyu akiwa na begi limejaa t-shirts akitafuta wateja mitaa ya Jiji. Mfano wa sampuli alizo nazo ni kama hiyo aliyoivaa

DSCN0009 Hata katika mikutano ya chama, wapo wanao-take advantage

DSCN0138Vipo pia vibandiko kama hiki ambavyo hupatikana kwa sh 2000 

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO