Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Watu milioni 53 wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wanaishi chini ya mstari wa umaskini

Watu milioni 53 wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wanaishi chini ya mstari wa umaskini, hivyo juhudi za pamoja zinahitajika ili kuinua maisha yao.

Akiwasilisha matokeo ya ripoti ya 'Hali ya Afrika Mashariki 2012' iliyotolewa jana jijini Dar es Salaam, Ofisa Mradi wa taasisi ya Kimataifa ya Society for International Development (SID) Aidan Eyakuze, alisema asilimia 38 ya wananchi wa EAC ni maskini sana na kwamba nchini Tanzania idadi hiyo imeongeza kwa milioni 4.9 hadi kufikia milioni 14.9 kutoka milioni 10 katika kipindi cha 17.

Eyakuze alisema pamoja na ongezeko hilo kwa Tanzania, Kenya inaonekana kuwa na maskini wengi zaidi kwa kuwa na maskini milioni 18.9, Uganda (milioni 8.3) Burundi (milioni 6.3) na Rwanda (milioni 4.7).

"Chakula cha uhakika bado ni tatizo kubwa lakini jambo la kushangaza ni kwamba tuna ardhi nzuri na tunatumia mbolea kwenye kilimo chetu, swali linabakia ni kwa nini tuna njaa, kwa nini hatuwezi kulisha watu wetu?" alihoji.

Chanzo: Nipashe, Mei 25, 2012

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO