Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

TASWIRA ZA MKUTANO WA CHADEMA JANGWANI DAR ES SLAAM MEI 26, 2012

M4C Dar16

Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Mh Freeman Mbowe akihutubia mkutano mkubwa wa uzinduzi wa programu mpya ya chama chake ya Movement for Change (M4C) katika viwanja vya Jangwani Dar es Salaa jana. Alisema harakati za mabadiliko yanayofanywa sasa na chama hicho kupitia kaulimbiu yao ya (M4C) ni maandalizi ya kushika dola mwaka 2015 na kuwataka wananchi kushiriki kwa kila namna katika harakati hizo

M4C Dar15Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa akihutubia jana Jangwani, alisema taifa lipo katika hali ngumu ikiwamo, mfumuko wa bei, unaosababisha kupanda kwa gharama za maisha kunakochangiwa na na matumizi mabaya ya serikali.

M4C Dar17Mbunge wa Singida Mashariki na Mnadhimu wa Kambi ya Upinzania Bungeni, Mh Tindu Lissu akihutubia jana. Aliwataka wananchi kufahamu umuhimu wa Katiba na kuweza kutoa maoni yatakayohitimisha utawala wa kichifu nchini.

M4C Dar18   Mbunge wa Ubungo, Mh John Mnyika akihutubia wananchi jangwani jana. Mbowe, Dr Slaa na Lissu ndio walikuwa wazungumzaji wakuu wa mkutano huo. (Picha hizi za mwanzo zimepatikana kwa msaada wa Blog ya Kulikoni Ughaibuni)

M4C Dar4Sehemu ya umati wa watu waliojitokeza kwenye Mkutno wa CHADEMA katika viwanja vya Jangwani ambapo mamia ya watu walirudisha kadi zao za vyama vya awali nakujiunga na chadema katika muendeleo za programu yao mpya maarufu kama “Vuguvugu la Mabadiliko” – M4C

M4C Dar7

M4C Dar9Baadhi ya kadi za CCM na vyama vingine zilizorudishwa leo na kupatiwa kadi mpya za CHADEMA leo katika mkutano wa M4C Jangwani

M4C Dar5Kutoka kushoto, Mh Tundu Lissu, Mh Godbless Lema, Mh Ezekiel Wenje, Mh Joseph Mbilinyi (Sugu)

M4C Dar10Sugu, Mbunge wa Mbeya Mjini akighani mbele ya maelfu ya watu waliofurika viwanjani hapo leo

M4C DarMbunge wa Kawe (CHADEMA) na Waziri Kivuli wa Ardhi, Mh Halima Mdee akiwasili viwanja vya jangwani leo

M4C Dar8

M4C Dar6

M4C Dar2Mkurugenzi wa Halamshauri na Bunge CHADEMA, Ndg John Mrema akitambulisha mkutano

M4C Dar19Mwenyekiti wa CHADEMA, Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Mh Freeman Mbowe akisisitiza jambo mkutanoni hapo jana (Picha zote na Jackson Wilson Mataka)  

KWA PICHA ZA MATUKIO TOFAUTI ZAIDI UNAWEZA KUTEMBELEA BLOG ZA WANAHABARI EVARIST CHAHALI NA JOHN BUKUKU

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO