Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Naibu jaji mkuu wa Kenya apatikana na hatia

Nancy Baraza

Jopo maalum la majaji lililoteuliwa na rais Mwai Kibaki kuchunguza tuhuma zilizokuwa zinamkabili Naibu Jaji Mkuu wa Kenya Nancy Baraza kumdhalilisha mlinzi mmoja katika duka moja kubwa mjini Nairobi, imependekeza, jaji huyo kuondolewa madarakani.

Akisoma hukumu hiyo mjini Nairobi leo, mwenyekiti wa jopo hilo, Jaji mkuu mstaafu wa Tanzania, Augustino Ramadhan, amesema Nancy Baraza akiwa mtumishi wa chombo cha kusimamia sheria na haki hakutakiwa kwa namna yoyote kutenda kosa hilo dhidi ya mlalamikaji Bi Rebecca Kerubo.

Amesema kitendo alichofanya Nancy Baraza na ni cha utomvu mkubwa wa nidhamu na hivyo kupendekeza kwa Rais Mwai Kibaki kumwondoa katika wadhifa wake wa naibu jaji mkuu.

Nancy Baraza alituhumiwa kumnyanyasa na kumpiga Bi Kerubo tarehe 31 Desemba 2011, baada ya kutakiwa kufanyiwa ukaguzi kabla ya kuingia katika duka hilo, utaratibu ambao umekuwa ukitekelezwa kwa wateja wote.

Published by BBC Swahili on  6 Agosti, 2012

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO