Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

LOWASA AONGOZA VIONGOZI NA WANANCHI MAZISHI YA NYITI ARUSHA

Mh Lowassa akiongoza viongozi kwenda kwenda kuweka udongo kaburini,nyuma yake ni Waziri wa mambo ya nje Mh Bernard Membe.

Waziri Mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa ameongoza maelfu ya Wakati wa mji wa Arusha na mikoa ya jirani katika mazishi ya mfanyabiashara na Kanda maarufu wa CCM Mkoani Arusha Henry Nyiti,nyumbani kwake Tengeru Arusha.


Nyiti alifariki ghafla wiki iliyopita akiwa katika mgodi wake wa madini,Mahenge Mkoani Morogoro.


Wengine waliyoudhuria Ni pamoja na Waziri wa Mambo ya nje Bernard Membe,Naibu Waziri wa maliasili na utaalii Lazaro Nyalandu,mwenyekiti wa makampuni ya IPP Dr Reginald Mengi,Mkuu wa mkoa wa Arusha, mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe na Ridhiwani Kikwete.

Waziri Mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa pia alikwenda kutoa pole katika msiba wa Moja wa wazee maarufu eneo la Mto wa Mbu, mzee Athman.

Mwenyekiti wa chadema Freeman Mbowe akiweka udongo

Mh Lowassa akisalimiana na Mh Mbowe

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe akiweka shada la maua

PICHA ZOTE NA FATHER KIDEVU ‘MROKIM’

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO