Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

KAMPUNI YA MEGATRADE YATOA MSAADA WA SUFURIA KWA SHULE WENYE THAMANI YA ZAIDI YA SHILINGI MIL.2

DSCN0438

Kulia wa pili ni diwani wa kata ya Unga ltd Mh.Issa Saidi akisalimiana na Afisa masoko na matukio wa kampuni ya Megatrade Jailos Joseph kama ishara ya shukrani baada ya kampuni hiyo kukabidhi msaada wa sufuria mbili  kwa shule ya Msingi Ungaltd zenye thamani ya zaidi ya shilingi Mil.2 kulia wa kwanza aliyevalia kitenge ni Ester Rodrick – Afisa Elimu Kata ya unga ltd,kushoto ni Joachim Kisarika – Afisa Mtendaji kata ya unga ltd na Kakwaya Ruji  – Afisa wa shughuli maalum za Megatrade Inv. ltd

DSCN0441

Hapa picha ikionyesha wafanyakazi wa Megatrade pamoja na uongozi wa kata na shule wakiwa katika picha ya pamoja kushoto ni Happiness Kimaro ambaye ni secretari wa kampuni

Msaada huo umekuja baada ya uongozi wa kata pamoja shule kuandika barua kwa kampuni hiyo kuomba msaada wa sufuria mbili za ujazo wa lita 100 na lita 200 kwaajili ya kuwapikia chakula  wanafunzi wakiwa shuleni,  kutokana na wanafunzi kushinda njaa kwa muda mrefu na kushindwa kumudu masomo yao vizuri hali inayopelekea  wakati mwingine kuanguka na kupoteza fahamu na wengine kutoroka shule kutokana na njaa

Akikabidhi msaada huo kwa niaba ya kampuni Afisa masoko na matukio wa kampuni ya megatrade Bw Jailos Joseph alisema kuwa kampuni imeguswa na hali hiyo  ya wanafunzi kukosa chakula shuleni  na kusababisha baadhi yao kutoroka mchana au kushindwa kufwatilia vizuri masomo yao kutokana  na njaa huku akiweka wazi kuwa ukiwa na njaa huwezi kutuliza akili darasani na hivyo kuchangia kushuka  kwa ufaulu wa watoto katika mitihani yao.

Hata hivyo alisema kuwa  kampuni iliitikia wito huo  ikiwa ni sehemu ya mpango wake wa kurudisha kwa jamii kile kidogo kinachopata kutokana na kuuza bidhaa zake za K-Vant Gin na Kiroba Original ikatoa sufuria hizo 2 za ujazo wa lita 200 kila moja zenye thamani ya zaidi ya 1,200,000 ili kunusuru hali ya elimu katika kata hiyo ya unga ltd na taifa kwa ujumla.

Kwa upande wa Kata, Diwani alisema wanafanya utaratibu wa mkutano wa kamati ya shule , kata, wazazi na wanafunzi wote kuwaonyesha na kuwakabidhi msaada huu ambapo watawaita  na kututambulisha kwao, kuwa wao ndo waliotoa  msaada huo huku akitoa neno la shukrani kwa kampuni ya Megatrade  kwa niaba ya kata na shule

DSCN0442

PICHA NA STORI: PAMELA MOLLEL

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO