Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Tamasha la Michezo kwa vijana wa Arusha kufanyika Jumamosi Machi 30, 2013 Viwanja vya Soweto; Kiingilio ni Bure!

DSCN7333Waratibu wa bonanza la vijana Jijini Arusha linalotarajiwa kufanyika Machi 30, 2013. Sayuni Wiliam, Immanuel na Mathias Paul wakizungumza na blog hii jana.

****************

Katika kuelekea sikukuu ya Pasaka, Vijana wa Jijini Arusha kupitia umoja wao ‘Vijana Kwa Pamoja Tunaweza’ kwa kifupi VIPATU wameandaa siku maalumu kujumuika pamoja kwa michezo mbali mbali sambamba na kupata wasaa wa kuwa karibu na viongozi wa kijamii Jijini hapa katika viwanja vya wazi Soweto.kuanzia saa 3 asubuhi.

Katika siku hiyo (Macho 30, 2013) inaelezwa kuwa kutakuwepo na michezo ya aina mbalimbali ikishirikisha makundi mbali mbali ya kijamii na kwamba kila mwananchi atakayehudhuria siku hiyo ataruhusiwa kushiriki mchezo atakaoupenda

Akizungumza na Blog Hii, Mratibu wa Bonanza hilo Doris Kessy amestaja baadhi ya michezo inayotazamiwa kushindaniwa siku hiyo ni pamoja na mpira wa miguu, mpira wa pete, kurusha vitu vizito, kukimbiza kuku na kukimbia na magunia.

Michezo mingine ni mpira wa kikapu, mbio za miguu mitatu, kukimbia na fimbo, sarakasi na kuruka kamba.

Doris anasema watu wote hususani vijana wa Arusha wanaalikwa kuhudhuria na kushiriki bonanza hilo la bure na kwamba majina ya washiriki wa michezo mbalimbali yataorodheshwa asubuhi viwanjani hapo siku ya bonanza.

Mratibu huyo aliwataja baadhi ya wadhamini ambao wamethibitisha kusaidia Bonanza hilo ni pamoja na Pepsi, Maezeki, Angaza, pamoja na Yes Tanzania.

Blog hii inafuatilia zaidi kuhusu Bonanza hili na kukujuza zaidi!

vipatu head

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO