Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Taswira za Mkutano wa UVCCM Uliofanyika jana Mjini Morogoro

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Taifa, Sadifa Hamis Juma akihutubia aktika mkutano wa UVCCM uliofanyika jioni hii kwenye Uwanja wa shule ya msingi Mkwajuni, Kata ya Kichangani mkoani Morogoro leo Machi 3, 2013, ikiwa ni mwisho wa ziara yake na viongozi wa kitaifa wa Jumuia hiyo mkoani humo, kukagua na kuimarisha uhai wa Chama na UVCCM

Mbunge wa Morogoro, Abdulazizi Mohammed Abood akieleza utekelezaji wa ilani ya CCM, baada ya kupandishwa jukwaani na Sadifa (wapili kushoto) wakati wa mkutano huo.

Sadifa akikabidhi kadi ya Umoja wa CCM, kwa mwanachama mpya wakati wa mkutano huo. Jumla ya wanachama 1700 walipewa kadi.

Sadifa na baadhi ya viongozi wakishirikina na wanachama kula kiapo cha CCM baada ya wanachama wapya wa UVCCM kupewa kadi kwenye mkutano huo

Katibu Mkuu wa UVCCM, Martine Shigela akihutubia kwenye mkutano huo

Mmoja wa vijana waiofukuzwa Chadema kwa kuhujumu chama na baadae kuhamia CCM, Mtela Mwampamba akihutubia kwenye mkutano huo.

"Vijana Chadema wanawazingua tu, wanawahamasisha kufanya maandamano ili wawapige picha za kwenda kuonyesha  nchi za nje kwa marafiki zao kwa ajili ya kupatiwa mamilioni ya fedha", anasema Mwampamba kwenye mkutano huo. Kulia ni Mkuu wa Utawala Makao Makuu ya UVCCM Kaka Mpokwa.

VIjana wakiwa wamembeba Mwampamba

 

Kama Mwampamba, Aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chadema (BAVICHA) Taifa, ambae pia alifukuzwa kwenye chama hicho kama Mwampamba na wenzake, Juliana Shonza, ambaye amehamia CCM hivi karibuni, akibebwa na vijana wa UVCCM, baada ya 'kuimwagia razi' Chadema jukwaani kwenye mkutano huo.

"Hawa walijaribu kuwapiga mawe ili msifike kwenye mkutano huu, lakini tazama mlivyofurika! Sasa ninasema, Uwezo wa kuwapiga tunao na nia ya kuwapiga tunayo..Tutawapiga, lakini sisi hatutawapiga kwa mawe ila kwa sera zetu makini" akasema Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro, Sixtus Mapunda wakati akihutubia kwenye mkutano huo.

Mbunge wa Morogoro, Abdulaziz Mohamed Abood akiongoza msafara wa pikipiki kwenda kwenye mkutano huo

Vijana wakiserebuka kwa nyimbo za hamasa kwenye mkutano huo

"Raaaaaaa UVCCM" Vijana hawa wa CCM wakati wa shamrashamra kwenye mkutano huo

Kujimwaya mwaya hakukukoma hadi mwisho wa mkutano.Picha zote na Bashir Nkromo-idara ya itikadi na uenezi CCM 

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO