Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

TASWIRA: UJUMBE WA CCM WAKIENDELEA NA ZIARA YAO GUANGZHOU NA DONGGUAN,NCHINI CHINA

Mtumishi katika mnara wa Canton, mrefu kuliko yote nchini China na watatu duniani kwa urefu, Sarah Xie, akimuonyesha mandhari ya jiji la Guangzhou, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, wakati Kinana na ujumbe wake walipopanda hadi mwisho mnara huo wenye urefu wa zaidi ya futi 100, Machi 13, 2013. Wengine Kulia ni Katibu wa CCM mkoa wa Mbeya Maganga Sengelema na Katibu Mkuu wa UVCCM, Martine shigella. Kinana na ujumbe wake wapo nchini kwa ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC).

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na ujumbe wake wakitazama maumbo ya mandhari ya mji wa Guanzhou, China, yaliyopo ndani ya mnara wa Cnton wenye urefu wa zaidi ya mita 100, walipotembelea mnara huo, Machi 13, 2013. Kinana na ujumbe wake wapo nchini kwa ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC).

Katibu wa NEC, Ushirikiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro (kushoto) na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa mjini Magharibi, Yussuf Mohamed Yusuf wakitaza bidhaa zinazouzwa kwenye kilele Mnara wa Canton ambao ni mrefu kuliko yote nchini China ukiwa na urefu wa zaidi ya mita 100, mjini Guangzhou, China. Dk. Asha-Rose Migiro na Yusuf ni miongoni mwa viongozi walioambatana na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana katika ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC).

Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akijaribu uzito wa spika, alipotembelea Kituo kikubwa cha Sayanasi na Teknolojia cha Ljieafun cha Guangzhou, kinachojihusisha na ubunifu na utengenezaji 'divaisi' za sauti na uchanganyaji ragi na matangazo kama ya biashara katika kumbi za muziki au vituo vya televisheni. Kulia ni Rais wa Kituo hicho, Mike Fung na wapili kulia ni Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, CCM, Dk. Asha-Rose Migiro. Kinana na ujumbe wake wapo nchini kwa ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC).

Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiwa katika mazungumzo na Kamishna wa maadili na nidhamu wa Chama Cha Kikomunisti cha China (PCP) jimbo la Dongguan, Cui Jian, kwenye hoteli ya Exibition International mjini Dongguan, China, Machi 13, 2013. Kinana na ujumbe wake wapo nchini kwa ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC).

Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akipewa zawadi na Kamishna wa maadili na nidhamu wa Chama Cha Kikomunisti cha China (PCP) jimbo la Dongguan, Cui Jian, kwenye hoteli ya Exibition International mjini Dongguan, China, Machi 13, 2013. Kinana na ujumbe wake wapo nchini kwa ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC).

Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimpa vipeperushi kuhusu utalii wa Tanzania, Kamishna wa maadili na nidhamu wa Chama Cha Kikomunisti cha China (PCP) jimbo la Dongguan, Cui Jian, kwenye hoteli ya Exibition International mjini Dongguan, China, Machi 13, 2013. Kinana na ujumbe wake wapo nchini kwa ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC).

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na Maofisa wa Mambo ya Nje wa Dongguan, China, Sarah Xie (kulia) na Sabina Liu, wakati wa chakula cha jioni kilichoandaliwa na Kamishna wa maadili na nidhamu wa Chama Cha Kikomunisti cha China (PCP) jimbo la Dongguan, Cui Jian, kwenye hoteli ya Exibition International mjini Dongguan, China, Machi 13, 2013. Kinana na ujumbe wake wapo nchini kwa ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC).

Katibu wa NEC, CCM, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, akizungumza na Maofiwa wa Mambo ya Nje wa Dongguan Sarah Xie (kulia) na Sabina Liu, wakati wa chakula cha jioni kilichoandaliwa na Kamishna wa maadili na nidhamu wa Chama Cha Kikomunisti cha China (PCP) jimbo la Dongguan, Cui Jian, kwenye hoteli ya Exibition International mjini Dongguan, China, Machi 13, 2013. Kinana na ujumbe wake wapo nchini kwa ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC).

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha Rose Migiro, wakiwa na viongozi wa Jumuia ya Watanzania waishio China, alipokutana nao Machi 12, 2013 kwenye hoteli ya Exhibition Internation mjini Dongguan, China. Kushoto ni, David Chamala (Katibu) na John Ruhembiza (Mwenyekiti) na kulia ni Abraham Merishan (Makamu Mwenyekiti) na Abubakar Mwinyi (Katibu Msaidizi). Kinana na ujumbe wake wapo nchini kwa ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC).

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO