Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

WAZIRI MKUU,MIZENGO PINDA, LOWASSA, WASSIRA NA NYALANDU WAMEFIKA KATIKA KANISA KATOLIKI LA MT.JOSEPH MFANYAKAZI, PAROKIA YA OLASITI,JIMBO KUU LA ARUSHA KUWAFAJIRI WAFIWA NA MAJERUHI

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Viongozi na Waumini wa Kanisa Katoliki la Olasiti Jijini Arusha May 7,2013 alikokwenda kutoa pole kufuatia mlipuko wa bomu la kutupwa kwa mkono uliotokea kanisani hapo May 6,2013 na kusababisha vifo na majeruhi.

Paroko wa Kanisa Katoliki la Olasiti la Arusha Peddy Castelino akiomba wakati Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alipotembelea kanisa hilo May 7,2013 kutoa pole kufuatia mlipuko wa bomu la kutupwa kwa mkono uliotokea kanisani hapo May 6,2013 na kusabisha vifo na majeruhi.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Paroko wa Kanisa Katoliki la Olasiti jijini Arusha, Peddy Castelino (kulia) May 7,2013 wakati alipotembelea kanisa hilo May 6,2013 ambako ulitokea mlipuko wa bomu la kutupwa kwa mkono na kusababisha vifo na majeruhi.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiangalia sehemu lilipodondoshwa bomu hilo.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwapa Pole Askofu wa Jimbo Kuu la Arusha, Mhashamu Josephat Lebulu (kushoto ) na Balozi wa Vatican nchini, Askofu Mkuu, Francisco Montecillo (katikati), May 7,2013 baada ya kutembelea Kanisa Katoliki la Olasiti jijini Arusha ambako May 6,2013 ulitokea mlipuko wa bomu la kutupwa kwa mkono na kusababisha vifo na majeruhi.

Paroko wa Kanisa Katoliki,Parokia ya Olasiti,Padri Peddy Costelino akitoa maelezo jinsi mlipuko ulivyotokea jana(katikati) ni Waziri wa Nchi ofisi ya Rais(Mahusiano)Stephen Wasira na Waziri Mkuu Mstaafu,Edward Lowassa

Waziri Mkuu Mizengo Pinda akimsikiliza Msaidizi wa Askofu Jimbo Kuu la Arusha,Simon Tenges

Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akilakiwa na Paroko wa Kanisa Katoliki,Parokia ya Olasiti,Padri Peddy Costelino

Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akisalimiana na viongozi

Paroko wa Kanisa Katoliki,Parokia ya Olasiti,Padri Peddy Costelino akizungumza

Paroko wa Kanisa Katoliki,Parokia ya Olasiti,Padri Peddy Costelino akizungumza

Waziri Mkuu mstaafu,Edward Lowassa akizungumza leo

Waziri wa nchi ofisi ya Rais(Mahusiano na Uratibu)akitoa salamu za pole

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii akitoa salamu zake

Mbunge wa Viti maalumu mkoa wa Arusha,Catherine Magige akitoa salamu zake

Waziri Mkuu Mizengo Pinda akitoa salamu za serikali kwa kuwataka wananchi kutoa taarifa zitakozoweza kuwatia mbaroni wahalifu

Viongozi mbalimbali wakiongozwa na Waziri Mkuu,Pinda wakiwa kwenye eneo la kanisa liliopotokea tukio la maafa ya mabomu

Wananchi wakimsikiliza Waziri Mkuu

Taasisi ya ujasusi ya Marekani(FBI)wameingia jijini Arusha kuchunguza tukio la ulipuaji wa Kanisa katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi,Parokia ya Olasiti jijini Arusha.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Magesa Mulongo ameyasema hayo jioni ya leo wakati akitoa taarifa kwa waziri Mkuu,Mizengo Pinda aliyefika kuwafariji wafiwa na kutoa tamko la serikali
Pinda amesema kuwa hakuna mtu atakayeweza kukomesha dini nyingine kwa kuua viongozi wa dini yeyote bali jambo linalitakiwa ni kuvumiliana watu wa imani tofauti na kuendelea kudumisha amani

Watu mbalimbali wanashikiliwa wakiwemo raia wanne wa Saudia Arabia ambao waliwasili nchini kupitia uwanja wa ndege wa Kilimanjaro(KIA)na kuondoka nchini kupitia mpaka wa Namanga wakielekea nchini Kenya baada ya tukio kutokea.

PICHA: OFISI YA WAZIRI MKUU; MAELEZO NA FILBERT RWEYEMAMU

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO