Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MAJINA YA WATUHUMIWA WANAOHOJIWA JUU TUHUMA ZA KULIPUA BOMU KANISANI ARUSHA HAYA HAPA!

Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha,Liberatus Sabas. PIcha na Filbert Rweyemamu


Arusha

Jeshi la Polisi linawashikilia na kuwahoji watuhumiwa 12 wanaodhaniwa kuhusika na tukio la mlipuko wa Bomu uliotokea katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Parokia ya Olasiti jijini Arusha jumapili iliyopita.

Akizungumza na waandishi wa habari leo,Kamanda wa Polisi mkoani hapa,Liberatus Sabas amesema upelelezi wa awali umekamilika na majalada ya watuhumiwa yamepelekwa kwa Mwanasheria wa serikali kwa hatua zaidi.

Amewataja wanaoshikiliwa na jeshi hilo kuwa ni Victor Ambrose Calist(20),Jeseph Yusuph Lomayani(18)waendesha Bodaboda wakazi wa Kwa Mrombo jijini Arusha, George Batholomeo Silayo(23)mfanyabishara na mkazi wa Olasiti,Arusha,Mohamed Sulemani Said(38)Mkazi wa Ilala,Dar es Salaam,Said Abdallah Said(28)raia wa Falme za Kiarabu.

Sabas aliwataja wengine kuwa ni Abdulaziz Mubarak(30)mkazi wa Abudhabi,raia wa Saudi Arabia,Jassini Mbaraka(29)mkazi wa Bondeni jijini Arusha,Foud Saleem Ahmed(28)mkazi wa Falme za kiarabu na Said Mohsen mkazi wa Najran,Falme za Kiarabu ambao bado wanaendelea kuhojiwa.

Wakati huo huo Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini ameahidi kutoa kiasi cha Sh 50 milioni kwa atakayetoa taarifa zitakazowezesha  kukamatwa kwa waliofanya kitendo hicho cha kigaidi.

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO