Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Chadema kidedea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Usa River - Arusha; wakomba mitaa 6, CCM waambulia mitaa 3

DSCN6121Mbunge wa Arumeru Mashariki, Mh Joshua Nassari akiwa kwenye gari ya wazi na wafuasi wa Chadema katika mji wa Usa River wakifurahia matokeo ya uchaguzi kuwatafuta wenyeviti wa Serikali za mitaa ambapo Chadema waliweza kuibuka kidedea kwa kujinyakulia uongozi wa mitaa 6 kati ya tisa iliyokuwa inagombaniwa. Katika uchaguzi huo uliofanyika jana huku mvua kubwa ikinyesha maeneo tofauti kiasi cha kuharibu mawasiliano kwa baadhi ya maeneo, ulishirikisha jumla ya vyama vitatu ambavyo ni CHADEMA, CCM na AFP ambao walishiriki mitaa miwili tu.
Kwa matokeo hayo ya viti sita kwenda CHADEMA, ni wazi kuwa nafasi ya kuongoza Halmashauri ya Mji mdogo wa Usa River itachukuliwa na chama hicho kwa maana kwamba tayari wanakura nyingi endapo kila chama kitapigia upande wake! Viti maalumu pia vinaweza kuongeza idadi ya kura za Chadema katika kumchagua meya wa Halmashauri ya Mji huo mdogo wa Usa River.
Chadema waliibuka washindi kwa kuchukua uenyekiti wa mitaa ya Mji Mwema, Kisambale, Manayata Kati na Banana.
Mitaa mingine ni Magadini na Ngarasero ambao ulielezwa kuwa ngome kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM katika mji huo.
CCM kwa upande wao waliweza kujinyakulia mitaa yaMlima Sioni, Magadirisho na Usa Madukani.
DSCN6120
DSCN6126
DSCN6123Shamrashamra za kushangilia ushindi
DSCN6101Mh Joshua Nassari akipokea matokeo ya awali kutoka vituo mbalimbali vya kupigia kura ndani ya Halmashauri ya mji mdogo wa Usa River kwa njia ya simu ndani ya kituo cha chama chake cha kufanya majumuisho ya kura kwa upande wa Chadema jana.
DSCN6103Hali ya barabara ilikuwa ni ya utelezi na matope sana kwa meoneo mengi ya mji
DSCN6110Mh Nassari akifurahia matokeo yaliyokipatia ushindi chama chake na baadhi ya viongozi wa chama na wadau wengine mahali walipojibanza barazani kukwepa mvua
DSCN6116Hapa Nassari alikuwa akiwafahamisha wananchi matokeo rasmi ya uchaguzi ambao walishiriki, baada ya kupata matokeo ya maeneo yote.
DSCN6100Gari iliyotolewa na mmoja wa madiwani wa Chadema mjini Arusha ili kusaidia kampeni hizo
DSCN6104Kabla ya matokeo ya jumla, CCM nao walionekana mitaani wakipita kwa shamrashamra kuanza kushangilia lakini furaha yao ilizimwa ghafla na matokeo ya mwisho baada ya kujikuta wameambulia mitaa 3 tu kati ya 9.
TAARIFA ZAIDI KUHUSU UCHAGUZI HUO KAMA ILIVYOANDIKWA NA GRACE MACHA WA TANZANIA DAIMA INAELEZA…..
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeendelea kudhihirisha umwamba wake katika Mkoa wa Arusha, ambapo kwa mara nyingine tena kimeipiga kikumbo CCM na kutwaa halmashauri mpya ya Mamlaka ya Mji Mdogo wa Usa River.
Ushindi huo unakuja zikiwa ni siku chache tangu chama hicho kiitwae Kata ya Daraja Mbili jijini Arusha ambayo ilikuwa ikiongozwa na diwani wa Chama Cha Mapinduzi, aliyefariki dunia.
Uchaguzi huo ulifanyika kutokana na Halmasuri ya Arumeru Mashariki kugawanywa, na hivyo kuunda halmashauri mpya ya mamlaka ya mji mdogo wa Usa River.
Kabla ya kugawanywa, mitaa yote ilikuwa ikiongozwa na CCM na hivyo, ikalazimika viongozi hao wajiuzulu ili uchaguzi ufanyike upya wa kuwapata wenyeviti wapya wa mitaa tisa.
Hadi tunakwenda mitamboni jana jioni, tayari CHADEMA kilikuwa kimejizolea ushindi mkubwa katika mitaa sita, huku CCM kiking’ara kwenye mitaa mitatu.
Mitaa hiyo na kura zake kwenye mabano ilikuwa Manyata Kati (CHADEMA 118, CCM 78), Nganana (CHADEMA 127, CCM 117), Kisambare (CHADEMA 613, CCM 190), Ngarasero (CHADEMA 785, CCM 355) na Magadini ambako CHADEMA walipata kura 303 dhidi ya 106 za CCM.
Hata hivyo, CCM ilifanikiwa kurejesha mitaa mitatu ya Magadirisho, Mlima Sioni na Usa Madukani.
Kwa ushindi huo, CHADEMA sasa wamefanikiwa kuongoza halmashauri ya pili katika Mkoa wa Arusha, kwani kwa zaidi ya miaka kumi wamekuwa wakiongoza Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.
Akizungumza na Tanzania Daima kwa simu jana, Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Arusha, Amani Golugwa, alisema kuwa wanataka kuifanya halmashauri mpya ya Usa River iwe ya mfano katika Jiji la Arusha.
“Tumejipanga kuiboresha Usa River kuanzia usafi, mapato na miundombinu yake, kwani CCM wamekuwa wakisuasua, lakini sasa wameachia,” alisema.
CHADEMA kimekuwa kikitoa ushindani mkubwa kwa CCM katika Mkoa wa Arusha kwani hata kwenye uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Arumeru Mashariki, chama hicho kilitwaa kiti hicho kilichokuwa kikikaliwa na wapinzani wao baada ya aliyekuwa mbunge kufariki.










Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO