Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

KINANA KUHUTUBIA ARUSHA LEO

CHAMA cha mapinduzi(CCM) mkoani Arusha kinataraji kumpokea  na kumkaribisha nyumbani katibu mkuu mteule wa CCM taifa, Abdulraham Kinana leo katika uwanja mdogo wa ndege uliopo Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha ambapo pia atapata fursa ya kuwahutubia wafuasi wa chama hicho mkoani Arusha katika uwanja wa kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid, sanjari na kufungua mashina mbalimbali ya wakereketwa.

Katika ziara hiyo Kinana ataambatana na katibu wa itikadi na uenezi,Nape Nnauye, Naibu Katibu Mkuu wa CCM bara, Mwigulu Nchemba pamoja na wajumbe mbalimbali wa sekretarieti mpya ya CCM ambapo  wanataraji kuongoza mashambulizi ya kushambulia ngome ya Chadema.

Katibu wa siasa na uenezi wa CCM mkoani Arusha, Isaac Kadogoo alisema  mkutano huo utafanyika leo sambamba na kufungua matawi na maandamano makubwa ya kumpokea Kinana kuanzia uwanja mdogo wa ndege Kisongo hadi wilayani Arumeru na kisha kurejea katikati ya jiji la Arusha.

Kadogoo alisema kwamba lengo la shughuli hiyo ni kumkaribisha Kinana ambaye ni mkazi wa mkoani Arusha sanjari na kuelezea sera mbalimbali yakiwemo maendeleo yaliyoletwa na CCM mkoani Arusha na nchini kwa ujumla.

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO