Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

ONESHO LA VAZI LA KHANGA ZA KALE LILIVYOFANA DAR

Mgeni Rasmi katika Onyesho la Khanga za Kale,Waziri wa Maendeleo ya Jamii,Jisnia na Watoto,Mh, Sophia Simba  akisoma hotuba yake fupi wakati wa kufungua rasmi Onyesho la Mavazi ya Khanga za Kale linaloratibiwa na Mamaa wa Mitindo,Asia Idarous Khamsin (kushoto) chini ya Kampuni yake ya Fabak Fashion.Onyesho hilo limefanyika usiku huu katika Hoteli ya Serena,Jijini Dar es Salaam.

Muandaaji wa Onyesho la Mavazi ya Khanga za Kale,Mamaa wa Mitindo,Asia Idarous Khamsin akizungumza machache kabla ya kuanza Rasmi kwa Onyesho hilo lililofanyika usiku huu katika Hoteli ya Serena,Jijini Dar es Salaam.

Washiriki wa Shindano la Unique Model,wakiwa Jukwaani wakati wakipita kuonyesha vazi hilo la Khanga za Kale.

Baadhi ya Wanamitindo wakipita Jukwaani kuonyesha mavazi ya aina Mbali mbali yaliyobuniwa na Wabaunifu zaidi ya 30 walioshiriki kuonyesha mavazi yao katika Onyesho hilo.

Mzee Khamsin na Mama Asia Idarous Khamsin wakipita jukwaani kutoa shukrani.

Mtaalam wa Vazi la Ghanga akitoa Somo.

 Pongezii....

 Wageni wa aina mbali mbali na kutoa sehemu mbali mbali pia walikuwepo kwenye Onyesho hilo. 

Ilifika wakati wa Kutoa Tuzo za Shukrani,ambapo Mama Ankal (kulia) alipokea Tuzo ya Globu ya Jamii.

 Mkurugenzi wa Prime Time,Juhayna Kussaga akipokea Tuzo kwa niaba ya Clouds TV.

 Mwanalibeneke Othman Michuzi wa Libeneke la MTAA KWA MTAA BLOG,akipokea Tuzo ya Blog yake kwa Mchango mkubwa aliounyesha juu ya Shindano hilo.

 Ankal Issa Michuzi akipokea Tuzo kwa niaba ya Blog ya Jiachie ambayo ipo chini ya Michuzi Jr.

 Misie Popular pia alilamba nondozz yake.

PICHA ZOTE: KWA HISANI YA WOINDE SHIZA (LIBENEKE LA KASKAZINI BLOG)

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO