Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Jaji Mkuu Mohamed Chande Othman ajitoa katika kesi ya ubunge ya Godbless Lema

JAJI Mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande Othman, amejitoa katika kesi inayomkabili aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.

Habari za kuaminika zilizopatikana mjini Dar es Salaam jana, zinasema Jaji Chande amejitoa na nafasi yake imechukuliwa na Jaji Bernard Luhanda, ambaye atashirikiana na Natalia Kimaro na Salum Massati, kusikiliza rufani hiyo namba 47/2012 ya mwaka 2012.

Hii ni mara ya pili, kwa Jaji kujiondoa, baada ya Jaji Mbarouk Salim Mbarouk kuwahi kujitoa.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Lema alikiri kupata taarifa za kujitoa kwa Jaji Chande.

“Nimepokea taarifa ya kujitoa kwa Jaji Chande, sijui sababu ni nini… hii ni mara ya pili kwa jaji kujitoa, najiuliza maswali mengi nakosa majibu, …unajua kesi hii si yangu, ni wananchi ambao wanashauku kubwa ya kutaka kujua hatma yangu,” alisema Lema.

Alisema baada ya kusikia taarifa hiyo, aliwasiliana na wakili wake Method Kimomogolo, ambaye alimthibitishia kujiondoa kwa Jaji Chande.

Rufaa hiyo itasikilizwa saa tatu asubuhi na jopo la majaji watatu, Nathalia Kimaro, Salum Massati na Jaji Benard Luanda wa Mahakama ya Rufaa.

Novemba 8, mwaka huu Mahakama ya Rufani ilimwamuru Lema kufanya marekebisho ya dosari za kisheria katika muhtasari wa hukumu ndani ya siku 14, kutokana na pingamizi lililowekwa na wajibu rufaa.

Mrufani huyo alishawasilisha rufaa hiyo upya, baada ya kufanya marekebisho na tayari imepangwa kusikilizwa wiki ijayo.

Awali rufaa hiyo ilikuwa ikisikilizwa na jopo la majaji watatu, Jaji Mkuu, Mohamed Chande Othman, Jaji Salum Massati na Jaji Nathalia Kimaro, ambapo kwa wiki ijayo hatokuwepo Jaji Othman, nafasi yake itachukuliwa na Jaji Luanda.

Lema alivuliwa wadhifa huo na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, Aprili 5, 2012 kufuatia kesi iliyofunguliwa na wanachama watatu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mussa Mkanga, Happy Kivuyo na Agnes Mollel, wakipinga ushindi wake katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2010.

Baada ya kushindwa, Lema alikata rufaa Mahakama ya Rufani, kupitia kwa wakili wake Method Kimomogoro kupinga hukumu ya Mahakama Kuu, huku akitoa hoja 18 za kupinga hukumu hiyo.

Chanzo:  Gazeti la Mtanzania, Nov 29, 2012 kupitia Jamii Forums

******

GAZETI MWANANCHI LIKAANDIKA HIVI
JAJI Mkuu wa Tanzania, Mohamed Othman Chande amejitoa kusikiliza rufaa ya kesi ya aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, badala yake nafasi yake imechukuliwa na Jaji Bernard Luanda.

Kujitoa kwa jaji mkuu kumekuja ikiwa zimebaki siku tano kusikilizwa upya kwa rufaa hiyo Desemba 4, mwaka huu, baada ya awali Mahakama ya Rufani, kuona rufaa hiyo ilikuwa na dosari.

Mahakama hiyo ilikubali hoja ya wajiburufaa kuwa rufaa hiyo ilikuwa na dosari kutokana na tofauti ya vifungu vya sheria vilivyotumika katika hukumu iliyomvua ubunge Lema na vilivyotumika katika hati ya kukaza hukumu, iliyowasilishwa mahakamani sambamba na rufaa hiyo.

Hata hivyo, kilichomwokoa Lema ni kifungu cha 111 cha Kanuni za Mahakama, ambapo mahakama hiyo ilisema kuwa chini ya kanuni hiyo, dosari hizo zinaweza kurekebishwa.

Jaji Chande ndiye aliyekuwa kiongozi wa jopo la majaji watatu katika kesi hiyo akiwamo Salum Massati na Natalia Kimaro.

Jaji Mkuu aliingia kwenye kesi hiyo akichukua nafasi ya Jaji Mbarouk Salim Mbarouk aliyekuwa amepangwa awali, ambaye sababu za kuondolewa hazikuwekwa wazi.

Wakili wa  Lema, Method Kimomogoro alithibitisha kuwa amepata taarifa kuwa jaji mkuu hatasikiliza rufaa hiyo na badala yake Jaji Luanda ndiye atachukua nafasi yake.

“Ni kweli jaji mkuu hatakuwapo kusikiliza rufaa ya Lema nimewasiliana na Msajili Dar es Salaam ameniambia hatokuwepo kwenye hilo jopo,” alisema Kimomogoro na kuongeza:

Hata hivyo, Wakili Kimomogoro alisema “Huu ni utaratibu wa kawaida wa mahakama kwa kuwa huenda jaji mkuu akawa amesafiri au ana shughuli nyingine.”

Wakili wa wajiburufaa, Alute Mughwai alisema hajapata taarifa kama Jaji Mkuu ameondolewa kwenye jopo hilo kwa kuwa huo si utaratibu wa mahakama kutoa taarifa hizo.

“Mahakama huwa haitoi taarifa, zinawekwa (taarifa) kwenye ubao wa mahakama siku ambayo rufaa inasikilizwa,” alisema.

Aliendelea, “Jaji yeyote atakayepangwa sisi hatuna tatizo kwa kuwa wote ni majaji, wewe uko huko Dar na mimi niko huku bara (Arusha), hivyo unaweza ukazipata taarifa zaidi huko kwa kuwa ndiyo uko jikoni Dar.”

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO