Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

CHADEMA wahitimisha kampeni za uchaguzi wa mitaa 9 mji mdogo wa Usa River kwa kishindo; Uchaguzi ni leo!

DSCN6047Kutoka kushoto, Mbunge wa Arumeru Mh Joshua Nassari, aliekuwa Mbunge wa Arusha Mjini Mh Godbless Lema, Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Arusha, Mh Amani Golugwa na Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa Mh John Heche wakiwa sehemu ya wageni muhimu katika mkutano wa hadhara kufunga kampeni za kuwania nafasi ya kuongoza mitaa tisa katika Halmashauri ya Mji mdogo wa Usa River – Arumeru Mashariki.
Kampeni hizo za Chadema zilihitimishwa jana katika uwanja wa Shule ya Msingi Usa ambapo wananchi walijitokeza kwa wingi sana. Leo Jumapili Novemba 4, 2012 uchaguzi huo unafanyika, na kwa mujibu wa Katibu wa Chadema Mkoa, Amani Golugwa, Chadema wamedai kujipanga kushinda mitaa yote sita ili kuweza kumsaidia Nassari ambae ni mbunge kutoka chama hicho kufanikisha utekelezaji wa mipango yake ya maendeleo kama Mbunge wa Jimbo hilo.
DSCN6058
Kwa siku ya jana Chadema walifanikiwa kufanya mikutano mingine minne ya kawaida maeneo tofauti ya Mji wa Usa chini ya Ally Bananga ambae alitokea kuwa kivutio kwa watu wengi, akisaidiana na Mbunge wa Arumeru Mashariki Mh Joshua Nassari kabla ya kuhitimisha kwa mkutano mkubwa katika viwanja hivyo vya shule ya Msingi Usa.
DSCN6061Mbunge wa Arumeru Mashariki, Mh Joshua Nassari akiongea na wananchi katika mkutano wa jana Usa River na kuwataka wananchi hao wamsaidie kupata viongozi hao wa mitaa watakaomsaidia kukamilisha ahadi mbalimbali za kuboresha maisha ya watu wake Jimboni humo.
DSCN6036Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa, John Heche akihutubia katika kutano huo ambapo aliwataka wananchi hao kutopoteza nafasi hii adimu ya kumuongezea nguvu Mbunge wao Joshua Nassari (CHADEMA) kwa kumchagulia wagombea hao wa tisa wa Chadema  kumsaidia.
DSCN6041Mbunge Joshua Nassari akiwasili viwanjani hapo na kulakiwa na wananchi kwa shangwe kama picha inavyoonesha.
DSCN6053Katibu wa Chadema Mkoa wa Arusha, Amani Golugwa akisisitiza jambo katika mkutano huo jana
DSCN6076Godbless Lema, ambae uamuzi wa rufaa yake unatarajiwa kutolewa baadae Novemba 8, 2012 Mahakama kuu Jijini dar es Salaam, nae alipata wasaa wa kuzungumza katika kkutano huo.
DSCN6078Mdau wa Blog hii akiteta jambo na Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Arusha, Amani Golugwa wakati mkutano unaendelea jana katika uwanja wa Shule ya Msingi Usa River
Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO