Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Daudi Kilo, Kamanda wa Chadema aliyewazawadia ‘lunch box’ watoto 384 wa shule za msingi wanaofanya mitihani ya kumaliza darasa la saba Mkoa wa Manyara

DSC05613

DSC05638

DSC05616

DSC05635

DSC05607

DSC05636

DSC05625

DSC05631

Katika picha tofauti anaonekana Daudi Kilo (mwenye koti la ledha), kamanda wa Chadema kutoka Handeni Tanga akiwa na baadhi ya wanafunzi na walimu wa Shule za Msingi zilizopo katika Wialaya za Karatu na Babati Vijijini baada ya kuwakabidhi zawadi mbali mbali jumla ya wanafunzi 384 waliokuwa wanajiandaa kuanza mitihani ya kumaliza Darasa la saaba mwaka huu.

Daudi Kilo alifanya ziara katika shule za msingi Bashay, Njia Panda, Rhotia na Jushi zilizopo Wilayani Karatu, pamoja na shule ya Tarangire iliyoko babati Vijijini.

Katika ziara hiyo aliambatana na mtu mwingine aliemtambulisha kwa jina la Chris Mbajo, na wote ni wanachama wa Chadema.

Kwa mujibu wa Daudi, aliamua kuwazawadia watoto hao vifaa mbalimbali vya kusomea kwa watoto hao ili kuonesha mapenzi yake kwa Tanzania na namna anavyothamini elimu kwa vijana hasa katika karne hii ya sayansi na teknolojia. Pia kuwaandaa kisaikolojia watoto hao kwa ajili ya mitihani waliyokuwa wafanye kesho yake.

Mbali na ‘lunch box’ hiyo, kila mtoto aliebahatika kupata zawadi za kamanda huyo, alijipatia pia peni, penseli, rula, note book, na ufutio. Pia kulikuwa na ndoo na mabeseni ya kuchotea maji na kunawia. Hii ilifanyika siku moja kabla ya kuanza mitihani yao

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO