Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA JUKWAA LA MAPINDUZI YA KIJANI

TANZANIA inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Jukwaa  la mapinduzi ya  kijani  Afrika( AGRF)  utakaofanyika kuanzia  septemba 26 hadi septemba 28 mjini Arusha  utakaokutanisha viongozi  mbali mbali wa  kimataifa  ambao  watajadili namna ya kuchukua hatua katika kuboresha usalama wa chakula duniani .

Aidha katika mkutano huo viongozi hao wataweza kujadili  sera ya mapinduzi ya kilimo na uchumi wa Afrika ,njia za kukuza masoko pamoja na namna ya kubadilisha mfumo wa kilimo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa Rais wa umoja wa mapinduzi ya kijani Afrika (AGRA) bi Jane  Karuku  alisema kuwa mkutano huo ni hatua inayofuata katika kuendeleza bara  la Afrika kupata ufumbuzi katika masuala ya usalama wa chakula.

Karuku alisema kuwa Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano huo katika kukuza sekta ya ukuaji wa kilimo inawakilisha uchunguzi  uliofanywa katika wilaya ya kilombero mkoa wa morogoro juu ya njia bora za kilimo.

Alieleza kuwa uchunguzi huo uliwezesha uzalishaji wa mahindi kwa wakulima wadogo wa wilaya hiyo kuongezeka kutoka tani 1.5 hadi 4.5 kwa hekta ,ambapo kwa upande wa mavuno ya mpunga yaliongezeka kutoka tani 2.5 hadi tani 6  hali iliyopelekea Tanzania kupata fursa hii  ya kuwa mwenyeji wa mkutano huo.

Aidha alisema kuwa jukwaa hilo litatoa nafasi ya kujadili namna bora ya kuendeleza mipango ya uwekezaji wenye tija kwa ajili ya kuongeza  maendeleo ya kilimo barani Afrika pamoja na kujadili namna bora ya kuunganisha nguvu ya jamii na sekta binafsi katika kuboresha usalama wa chakula duniani

Aliongeza kuwa jukwaa hilo pia litaweza kujadili na kutafuta njia bora za kuboresha kilimo barani Afrika na kuwawezesha wakulima wadogo wadogo  kushirikiana na vyama vya ushirika na wadau wengine ambapo mjadala huo utatoa njia bora za matumizi ya rasilimali na kukabiliana na changamoto zinazowakabili  mamilioni ya wakulima barani Afrika.

“Wakulima wadogo wadogo ni kitovu kwa yale yote tuyafanyayo hivyo mtazamo wetu ni kuwapatia wakulima wa afrika dhana za kilimo wanazohitaji ili waweze kukua zaidi na kuongeza kipato chao na watatuongoza katika kupata mafanikio mazuri”Alisema bi Jane.

Hata hivyo aliwataja viongozi wa kimatiafa watakaoudhuria mkuano huo kuwa ni pamoja Melinda Gates mwanzilishi wa co-melinda Gates rais wa IFAD Dk Kanayo Nwanze ,waziri wa kilimo wa Nigeria Dk Akinwumi Adesina ,mshindi wa tuzo ya chakula Prof .Gebisa Ejeta pamoja na rais wa shirika la kimataifa la Yara International Jorgen Ole Haslestad.

Source: Bashir Nkoromo; Imeandikwa na Rose Jackson, Arusha

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO